African Storybook
Menu
Nyani walioenda huku na huko
Brigid Simiyu
Benjamin Mitchley
Kiswahili
Watu wa kijiji cha Udongo walikumbwa na matatizo mengi.

Walihuzunika kwa sababu wanyama pori waliyahatarisha maisha yao.
Wanyama hao waliila mimea yao yote na kuwaiba watoto.

Mahali hapo hapakuwa pazuri pa kuishi tena.

Lakini, wangehamia wapi?
Watu wa familia moja walihamia milimani.

Waliamini kuwa wangepata chakula huko.
Milimani, kulikuwa na vichaka, mapango na miti mingi.

Walikula sungura na ndege.
Familia zingine ziliona jinsi familia ya milimani ilivyoishi vizuri.

Mtu mmoja aliwashawishi, "Maisha ya milimani ni mazuri. Nanyi hamieni huku."
Familia zingine zilihamia milimani.

Ziliishi mapangoni kulikokuwa na joto na usalama.
Watoto wa familia za milimani walizoe kupanda miti kutafuta matunda.

Walining'inia kwenye matawi kama vile kima hufanya.
Kadri muda ulivyopita, ndivyo familia za milimani zilivyobadilika kimaumbile. Watoto wao walipunguza maongezi yao wakawa wanakoroma zaidi.

Mapua ya watu wazima yalianza kuwa makubwa na waliota nywele zaidi kwenye miili yao.
Kila walipotazamana, waliona kwamba meno yao yaliendelea kuwa marefu.

Walianza kutembea kwa miguu minne.
Waligeuka wakawa viumbe wapya wasiokuwa wameonekana pahali pale mbeleni.

Wakaitwa nyani.
Mwanzoni, nyani hao waliishi kwa furaha.

Badala ya kula sungura, walianza kuyala mabuu.
Walisahau jinsi ya kutembea wima kama ilivyokuwa awali.

Wakavua nguo zao kwa sababu miili yao sasa ilikuwa imefunikwa kwa manyoya meusi.
Hata hivyo, walikumbuka kwamba walikuwa watu mbeleni.

Walipoyaona mapua yao makubwa, walichekana.
Baadaye, walianza kukasirishwa na tabia zao wenyewe. Walipochekana, waliruka juu na chini kwa hasira.

Vita vilizuka baina ya nyani hao wakalazimika kutawanyika.
Hiyo ndiyo sababu hata leo, nyani huishi katika makundi madogo na wala hawaishi kama taifa la nyani.
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Nyani walioenda huku na huko
Author - Southern African Folktale
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Benjamin Mitchley
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs
© African Storybook Initiative 2014
Creative Commons: Attribution 4.0
Source www.africanstorybook.org
Menu
  • Navigate

    Navigate through the story by swiping right or left or clicking when the cursors changes to an arrow on the right or the left edge of the screen.

    Tap or click on the centre of the page to see, or remove the menu bars at the top and the bottom of the screen. You can also use the ESC key.

    You can use the slider at the bottom as a way to move quickly through the story. On a mobile device tap on the slider before you drag the slider button.

    Click or tap to return to African Storybook.

  • Share
    If you have a Twitter or Facebook account, you can share this story on your page or a page you manage. You can also copy the web link (URL) for this story.
    • Twitter
    • Facebook
    • Url
  • Rate
    Other visitors rated this story

    Tell us how much you liked the story – drag the scroller to highlight one or more stars
    • Submit
  • Comment
    Read other people’s comments on the story, or add your own.
    • Enter your comment
    • Name
    • E-mail
    • Post
  • Translations and adaptations
    • The baboons that went this way and that
      English (Original)
    • The baboons that went this way and that
      English (Adaptation)
    • They Became Baboons
      English (Adaptation)
    • Les babouins qui vont çà et là
      French (Adaptation)
    • Izimfene ezaziya le na le
      isiZulu (Translation)
    • Tsingukye Tsitsakyeendaana Eyi Ni Neeyi
      Lumasaaba (Translation)
    • Enguge Ejerwenga Eno Ni Neera
      Lunyole (Translation)
    • Enguge Ejerwenga Eno Ni Neera
      Lunyole (Adaptation)
    • Ditšhwene tšeo di be go di e ya kua le kua
      Sepedi (Translation)
    • Ditshwene tse ileng tsa hasahana
      Sesotho (South Africa) (Translation)
  • Download to read
    Landscape version
  • Download to print
    Portrait (booklet) version
  • Download EPUB