Nyani walioenda huku na huko
Southern African Folktale
Benjamin Mitchley

Watu wa kijiji cha Udongo walikumbwa na matatizo mengi.

Walihuzunika kwa sababu wanyama pori waliyahatarisha maisha yao.

1

Wanyama hao waliila mimea yao yote na kuwaiba watoto.

Mahali hapo hapakuwa pazuri pa kuishi tena.

Lakini, wangehamia wapi?

2

Watu wa familia moja walihamia milimani.

Waliamini kuwa wangepata chakula huko.

3

Milimani, kulikuwa na vichaka, mapango na miti mingi.

Walikula sungura na ndege.

4

Familia zingine ziliona jinsi familia ya milimani ilivyoishi vizuri.

Mtu mmoja aliwashawishi, "Maisha ya milimani ni mazuri. Nanyi hamieni huku."

5

Familia zingine zilihamia milimani.

Ziliishi mapangoni kulikokuwa na joto na usalama.

6

Watoto wa familia za milimani walizoe kupanda miti kutafuta matunda.

Walining'inia kwenye matawi kama vile kima hufanya.

7

Kadri muda ulivyopita, ndivyo familia za milimani zilivyobadilika kimaumbile. Watoto wao walipunguza maongezi yao wakawa wanakoroma zaidi.

Mapua ya watu wazima yalianza kuwa makubwa na waliota nywele zaidi kwenye miili yao.

8

Kila walipotazamana, waliona kwamba meno yao yaliendelea kuwa marefu.

Walianza kutembea kwa miguu minne.

9

Waligeuka wakawa viumbe wapya wasiokuwa wameonekana pahali pale mbeleni.

Wakaitwa nyani.

10

Mwanzoni, nyani hao waliishi kwa furaha.

Badala ya kula sungura, walianza kuyala mabuu.

11

Walisahau jinsi ya kutembea wima kama ilivyokuwa awali.

Wakavua nguo zao kwa sababu miili yao sasa ilikuwa imefunikwa kwa manyoya meusi.

12

Hata hivyo, walikumbuka kwamba walikuwa watu mbeleni.

Walipoyaona mapua yao makubwa, walichekana.

13

Baadaye, walianza kukasirishwa na tabia zao wenyewe. Walipochekana, waliruka juu na chini kwa hasira.

Vita vilizuka baina ya nyani hao wakalazimika kutawanyika.

14

Hiyo ndiyo sababu hata leo, nyani huishi katika makundi madogo na wala hawaishi kama taifa la nyani.

15
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Nyani walioenda huku na huko
Author - Southern African Folktale
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Benjamin Mitchley
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs