Jimbi na Sungura
Ursula Nafula
Duane Arthur
Kiswahili


Hapo zamani za kale, kulikuwa na Jimbi na Sungura.
Walikuwa marafiki sana.
Walikuwa marafiki sana.
Usiku mmoja, Sungura aliitembelea familia ya Jimbi.
Walifurahia kula chajio pamoja.
Walifurahia kula chajio pamoja.
Walipolala, Sungura aligundua kitu fulani.
Jimbi na familia yake walivificha vichwa vyao walipolala.
Jimbi na familia yake walivificha vichwa vyao walipolala.
Jimbi na familia yake walilala fofofo.
Lakini, Sungura hakulala usiku kucha.
Lakini, Sungura hakulala usiku kucha.
Asubuhi walipoamka, Sungura alitaka kujua siri hiyo.
Akauliza, "Ninyi huviweka vichwa vyenu wapi mnapolala?"
Akauliza, "Ninyi huviweka vichwa vyenu wapi mnapolala?"
Jimbi, akitaka kumchezea shere Sungura, alimjibu, "Rafiki yangu, wakati wa kulala, sisi ndege huvikata vichwa vyetu ili tuweze kulala kwa starehe."
"Asubuhi tuamkapo, sisi huvirejesha vichwa vyetu mwilini," Jimbi aliendelea kueleza.
Sungura aliporudi nyumbani, aliwaelezea familia yake siri hiyo ya Jimbi.
Sungura waliamua kuijaribu siri hiyo wao wenyewe!
Unafikiri ni nini kilichotokea?
Sungura waliamua kuijaribu siri hiyo wao wenyewe!
Unafikiri ni nini kilichotokea?
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Jimbi na Sungura
Author - Geoffrey Thiiru
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Duane Arthur
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Duane Arthur
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs
© African Storybook Initiative 2015
Creative Commons: Attribution 4.0
Source www.africanstorybook.org
Creative Commons: Attribution 4.0
Source www.africanstorybook.org

