Jimbi na Sungura
Geoffrey Thiiru
Duane Arthur

Hapo zamani za kale, kulikuwa na Jimbi na Sungura.

Walikuwa marafiki sana.

1

Usiku mmoja, Sungura aliitembelea familia ya Jimbi.

Walifurahia kula chajio pamoja.

2

Walipolala, Sungura aligundua kitu fulani.

Jimbi na familia yake walivificha vichwa vyao walipolala.

3

Jimbi na familia yake walilala fofofo.

Lakini, Sungura hakulala usiku kucha.

4

Asubuhi walipoamka, Sungura alitaka kujua siri hiyo.

Akauliza, "Ninyi huviweka vichwa vyenu wapi mnapolala?"

5

Jimbi, akitaka kumchezea shere Sungura, alimjibu, "Rafiki yangu, wakati wa kulala, sisi ndege huvikata vichwa vyetu ili tuweze kulala kwa starehe."

6

"Asubuhi tuamkapo, sisi huvirejesha vichwa vyetu mwilini," Jimbi aliendelea kueleza.

7

Sungura aliporudi nyumbani, aliwaelezea familia yake siri hiyo ya Jimbi. 

Sungura waliamua kuijaribu siri hiyo wao wenyewe!

Unafikiri ni nini kilichotokea?

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Jimbi na Sungura
Author - Geoffrey Thiiru
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Duane Arthur
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs