African Storybook
Menu
Msitu wenye nyoka
Brigid Simiyu
Rob Owen
Kiswahili
Kijiji cha Sinyaire kimezungukwa na milima na misitu. Nyoka wengi huishi ndani ya misitu hiyo.

Wanakijiji walimwita Unyalego nyoka aliyekuwa mkubwa zaidi. Nyoka huyo aliwameza mbuzi na kondoo wakiwa wazima.
Siku moja, Apiyo, Ajoh na Atieno walienda msituni kutafuta kuni.

Bibi aliwaonya, "Jihadharini na Unyalego. Msichukue chochote kutoka msituni ila kuni."
Wasichana hao walifunganya maziwa, ndizi, viazi vitamu na maji.

Wakachukua kamba za kufungia kuni na panga kali.

Wakaondoka kwenda msituni.
Walipokuwa njiani, Ajoh, Apiyo na Atieno waliongea na kucheka.

Ghafla, Apiyo alisema, "Kimya! Tunakaribia anakoishi Unyalego."
Ajoh hakuzingatia onyo la bibi. Atieno aliwaita, "Tazameni, hapa kuna meno ya Unyalego ya dhahabu. Tuyachukue?"

Apiyo aliwakumbusha, "Msisahau kwamba bibi alituonya tusichukue chochote kutoka msituni ila kuni."
Ajoh akajibu, "Simwamini bibi. Nadhani alisema hivyo ili atuzuie kuchukua tunachotaka. Najua anatuonea wivu. Mimi nitayachukua hayo meno ya dhahabu."

Dada zake walikuwa na wasiwasi wakamwonya Ajoh lakini, hakujali.
Baadaye, Unyalego alikuja kutafuta meno yake. Alikasirika alipoyakosa.

Aliwasikia Ajoh, Apiyo na Atieno wakizungumza na kucheka.

Akajificha kando ya njia ambayo wasichana wale wangepitia.
Walipokwisha kuzikusnaya kuni, walizibeba vichwani. Ghafla, wakasikia "Hzzzzzzzzz!"

Walimwona Unyalego akiwa kinywa wazi, tayari kuwameza. Waliogopa sana wakajaribu kujificha.
Unyalego akawauliza, "Ni nani aliyeyachukua meno yangu ya dhahabu?" Walipokosa kumjibu, Unyalego akaamua kuwadadisi wasichana hao.

Akasema, "Ninataka muimbe wimbo. Yule atakayeimba bila kukosea, atakuwa hana hatia na ataenda nyumbani na kuni zake. Atakayekosea, ndiye aliye na hatia na atakuwa chakula changu kwa siku tatu zijazo!"
Apiyo aliimba kwanza kwa sauti nyororo:

Sio mimi, sio mimi niliyeiba meno, aliyeyaiba yuko hapo nyuma aaaah.

Kisha Atieno akaimba:

Sio mimi, sio mimi niliyeiba meno, aliyeyaiba yuko hapo nyuma aaaah.
Mwishowe, ilikuwa zamu ya Ajoh. Kwa uwoga alisongea mbele na kuanza kuimba:

S.i.o mi-mi, s.i.o. 

Aliimba vibaya akashindwa kuyatamka maneno sawa. Unyalego akamkemea, "Mbona huimbi vizuri kama wengine?"
Papo hapo, Unyalego akammeza Ajoh. 

Atieno na Apiyo walikimbia kuwaeleza wanakijiji yaliyotokea.
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Msitu wenye nyoka
Author - Joseph Sanchez Nadimo
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs
© African Storybook Initiative 2015
Creative Commons: Attribution 4.0
Source www.africanstorybook.org
Menu
  • Navigate

    Navigate through the story by swiping right or left or clicking when the cursors changes to an arrow on the right or the left edge of the screen.

    Tap or click on the centre of the page to see, or remove the menu bars at the top and the bottom of the screen. You can also use the ESC key.

    You can use the slider at the bottom as a way to move quickly through the story. On a mobile device tap on the slider before you drag the slider button.

    Click or tap to return to African Storybook.

  • Share
    If you have a Twitter or Facebook account, you can share this story on your page or a page you manage. You can also copy the web link (URL) for this story.
    • Twitter
    • Facebook
    • Url
  • Rate
    Other visitors rated this story

    Tell us how much you liked the story – drag the scroller to highlight one or more stars
    • Submit
  • Comment
    Read other people’s comments on the story, or add your own.
    • Enter your comment
    • Name
    • E-mail
    • Post
  • Translations and adaptations
    • Woud van slange
      Afrikaans (Translation)
    • Cisaka canzoka
      ChiTonga (Translation)
    • Sanga la Njoka
      CiNyanja (Translation)
    • Lul Thwol
      Dhopadhola (Translation)
    • Nyan ci kuec weet
      Dinka (Translation)
    • Forest of snakes
      English (Original)
    • The evil forest
      English (Adaptation)
    • Girl who did not listen
      English (Adaptation)
    • Forest of snakes
      English (Adaptation)
    • La Forêt Des Serpents
      French (Translation)
    • Insoka Isha Mumpanga
      IciBemba (Translation)
    • Insoka Isha Mumpanga
      IciBemba (Adaptation)
    • Ọhịa agwọagwọ
      Igbo (Translation)
    • Ihlathi leenyoka
      isiNdebele (Translation)
    • Ihlathi leenyoka
      isiXhosa (Translation)
    • Intombazana eyayinenkani
      isiXhosa (Adaptation)
    • Inyoka yehlathi, uMagilogilo
      isiZulu (Translation)
    • Irya mukuru
      Kinyarwanda (Translation)
    • Inzoka Kimizi
      Kinyarwanda (Adaptation)
    • Irya mukuru
      Kinyarwanda (Adaptation)
    • Asiyesikia la mkuu
      Kiswahili (Translation)
    • Omuwala owe mputtu
      Luganda (Translation)
    • Ekibira kye'Misota
      Lusoga (Translation)
    • Amoni Ang’Imunio
      Ng’aturkana (Translation)
    • Amoni Na Aya Ng'imunio
      Ng’aturkana (Adaptation)
    • Esichakha Esya Chinjukha
      Olunyala (Translation)
    • Omutsuru Kwe Tsinzukha
      Oluwanga (Translation)
    • Nandahulira
      Oluwanga (Translation)
    • A Floresta De Cobras
      Portuguese (Translation)
    • Eihamba ryenjoka
      Rukiga (Translation)
    • Ekibira ky'Enjoka
      Runyankore (Translation)
    • Lešoka la dinoga
      Sepedi (Translation)
    • Moru wa dinoha
      Sesotho (South Africa) (Translation)
    • Sekgwa sa dinoga
      Setswana (Translation)
    • Linoha Zamwa Mushitu
      SiLozi (Translation)
    • Mambakati, inyoka yelihlatsi
      Siswati (Translation)
    • Ḓaka ḽa dziṋowa
      Tshivenḓa (Translation)
    • Xihlahla xa tinyoka
      Xitsonga (Translation)
  • Download to read
    Landscape version
  • Download to print
    Portrait (booklet) version
  • Download EPUB