African Storybook
Menu
Magozwe
Ursula Nafula
Magriet Brink and Wiehan de Jager
Kiswahili
Katika jiji moja, kuliishi wavulana wa kurandaranda mtaani. Asubuhi moja walikuwa wakikoka moto kutumia karatasi walizookota.

Miongoni mwao alikuwepo Magozwe, aliyekuwa mdogo kuliko wote.
Wazazi wa Magozwe walifariki akiwa na umri wa miaka mitano tu. 

Magozwe alienda kuishi na mjombake ambaye hakumjali. Alifanya kazi nzito bila kupewa chakula.
Magozwe alipolalamika, mjombake alimpiga. Alipotaka kwenda shule, mjombake alisema, "Usinisumbue. Wewe ni mjinga. Hata huwezi kujifunza chochote."

Baada ya kuteswa kwa miaka mitatu, Magozwe alitoroka akaanza kuishi mtaani.
Maisha ya mtaani yalikuwa magumu. Walikosa chakula. Walikamatwa na polisi. Walichapwa na wananchi na pia walikuwa wagonjwa.

Mara kwa mara, kulikuwa na vita baina yao na makundi mengine. Wavulana hao walitegemea kuombaomba. Pia waliuza plastiki, vyuma, chupa na magazeti makuukuu.
Siku moja, Magozwe aliokota kitabu cha hadithi. Alikikukuta vumbi na kukiweka ndani ya gunia lake.

Kisha alizitazama picha kwani hakujua kusoma maneno.
Kitabu kilikuwa na picha za mvulana aliyekuwa rubani wa ndege. Magozwe alitamani sana kuwa rubani. Ndoto yake ilikuwa awe rubani bora zaidi ulimwenguni.

Mara nyingi aliyafumba macho na kuwaza kuwa alikuwa akiendesha ndege kubwa kuliko zote!
Ulikuwa msimu wa baridi. Magozwe aliombaomba barabarani. Mwanamume mmoja alimsalimu na kujitambulisha kwake, "Hujambo? Ninaitwa Tomaso. Ninapajua mahali unapoweza kupata chakula."

Tomaso alimwonyesha nyumba yenye paa la bluu. Magozwe alimtazama Tomaso, akaitazama ile nyumba kisha akasema, "Labda." Akaondoka na kwenda zake.
Miezi iliyofuata, wavulana wa mtaani walikuwa wamezoea kumwona Tomaso. Tomaso alipenda kuzungumza na watu walioishi mtaani. Aliwasikiliza wakizungumzia maisha yao. 

Tomaso alikuwa na nia nzuri, mvumilivu na mwenye heshima. Baadhi ya wavulana walianza kwenda katika nyumba ya paa la bluu. Wakati wa mchana walipata supu na mkate.
Magozwe alipokuwa akikitazama kitabu alichokiokota, Tomaso alimwuliza, "Hadithi hiyo inahusu nini?" 

Magozwe alimjibu, "Nadhani inamhusu mvulana aliyekuwa rubani."

"Anaitwaje?" Tomaso alimwuliza. Magozwe alijibu kwa sauti ya chini, "Sijui. Siwezi kusoma."
Baadaye, Magozwe alimweleza Tomaso sababu iliyomfanya atoroke kwa mjombake. Tomaso alimsikiliza ila hakumfanyia uamuzi.
Magozwe aliposherehekea miaka kumi ya kuzaliwa kwake, Tomaso alimpatia kitabu kipya cha hadithi. Kilimhusu mvulana mchezaji kandanda maarufu.

Tomaso alimsomea Magozwe hadithi hiyo kila mara. Siku moja alisema, "Wakati wa kwenda shule umefika. Utaweza kujisomea. Unaonaje?"

Tomaso alimwonyesa mahali watoto waliposaidiwa kwenda shule.
Magozwe alianza kufikiria kuhusu mahali hapo na kuhusu kwenda shule.

"Labda mjombangu alisema ukweli kwamba mimi ni mjinga na siwezi kujifunza chochote? Na je, nikipigwa huko nitafanyaje? Labda ni heri kubaki mtaani."

Magozwe aliyafikiria mambo hayo kwa hofu.
Magozwe alimwelezea Tomaso mawazo yake na hofu aliyokuwa nayo.

Muda ulipopita, Tomaso alimshawishi Magozwe. Alimwambia kuwa maisha yake yangekuwa bora iwapo ataenda shule.
Magozwe alihamia katika chumba kimoja kwenye jumba kubwa. Alikitumia chumba hicho pamoja na wavulana wengine wawili. Jumla, walikuwepo watoto kumi walioishi katika jumba lile.

Waliishi na Shangazi Cissy na mumewe, mbwa watatu, paka na mbuzi mmoja.
Magozwe alipoanza kwenda shule, haikuwa rahisi. Mara nyingi alitaka kukata tamaa.

Lakini, alipokumbuka rubani na mchezaji kandanda maarfu aliowasoma katika vitabu vya hadithi, alivumilia.
Siku moja Magozwe alipokuwa akisoma kitabu, Tomaso alimwuliza, "Hadithi unayoisoma inahusu nini?"

Magozwe alimjibu, "Inamhusu mvulana aliyekuwa mwalimu." "Anaitwaje?" Tomaso alimwuliza tena.

"Anaitwa Magozwe." Magozwe alisema kwa tabasamu.
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Magozwe
Author - Lesley Koyi
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Magriet Brink and Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - Read aloud
© African Storybook Initiative 2015
Creative Commons: Attribution 4.0
Source www.africanstorybook.org
Menu
  • Navigate

    Navigate through the story by swiping right or left or clicking when the cursors changes to an arrow on the right or the left edge of the screen.

    Tap or click on the centre of the page to see, or remove the menu bars at the top and the bottom of the screen. You can also use the ESC key.

    You can use the slider at the bottom as a way to move quickly through the story. On a mobile device tap on the slider before you drag the slider button.

    Click or tap to return to African Storybook.

  • Share
    If you have a Twitter or Facebook account, you can share this story on your page or a page you manage. You can also copy the web link (URL) for this story.
    • Twitter
    • Facebook
    • Url
  • Rate
    Other visitors rated this story

    Tell us how much you liked the story – drag the scroller to highlight one or more stars
    • Submit
  • Comment
    Read other people’s comments on the story, or add your own.
    • Enter your comment
    • Name
    • E-mail
    • Post
  • Translations and adaptations
    • Magozwe
      Afrikaans (Translation)
    • Magozwe
      Akuapem Twi (Translation)
    • ماقزوي
      Arabic (Translation)
    • Magozwe
      Asante Twi (Translation)
    • Magozwe
      ChiTonga (Translation)
    • Magozwe
      CiNyanja (Translation)
    • Magozwe
      Dagaare (Translation)
    • Magozwe
      Dagbani/Dagbanli (Translation)
    • Mokasa
      Dangme (Translation)
    • Magozwe
      English (Original)
    • Magozwe (Colour-in)
      English (Adaptation)
    • Magozwe
      Ewe (Translation)
    • Magozwe
      Fante (Translation)
    • Magozwe
      French (Translation)
    • Ankamafio
      Ga (Translation)
    • Magozwe
      Gonja (Translation)
    • Magozwe
      IciBemba (Translation)
    • UMagozwe
      isiNdebele (Translation)
    • UMagozwe
      isiXhosa (Translation)
    • Mhlaba ngiyakuhlonipha
      isiZulu (Translation)
    • Magozwe
      Kasem (Translation)
    • Magorwa
      Kinyarwanda (Translation)
    • Magozwe
      Kiswahili (Adaptation)
    • Magozwe apata makao mapya
      Kiswahili (Adaptation)
    • Magozwe
      Mampruli (Translation)
    • Magozwe
      Nzema (Translation)
    • Magozwe
      Portuguese (Translation)
    • Magozwe
      Sepedi (Translation)
    • Magozwe
      Sesotho (South Africa) (Translation)
    • Magozwe
      Setswana (Translation)
    • Magozwe
      SiLozi (Translation)
    • Wonkhe umuntfu uneliphupho
      Siswati (Translation)
    • Magozwe
      Talen (Translation)
    • Magozwe
      Tshivenḓa (Translation)
    • Mahewu
      Xitsonga (Translation)
  • Download to read
    Landscape version
  • Download to print
    Portrait (booklet) version
  • Download EPUB