African Storybook
Menu
Mvulana aliyechukiwa na wote
Brigid Simiyu
Wiehan de Jager
Kiswahili
Hapo zamani za kale, kulikuwa na mvulana mwenye sura mbaya sana.

Hakupendwa na yeyote, hata wazazi wake.

Hata nyumbani, aliketi peke yake wengine walipotazama runinga.
Shuleni pia aliketi peke yake watoto wengine walipokuwa wakicheza.
Walipokwenda kuwaleta mifugo, yeye alitembea nyuma yao.

Watoto wengine hawakutaka kutembea pamoja naye.
Alijua kuwa hakuna aliyemtaka wala kuzungumza naye.

Siku moja aliamua kutoroka, lakini hakujua pa kwenda.

Alitembea hadi kwenye msitu na kuanza kuogopa.
Alipokaribia msituni, alikutana na bibi mkongwe. Alikuwa mchafu na mwenye sura mbaya. Bi Kizee alimsalimia na kumwuliza, "Unafanya nini katika msitu huu wa kuogofya?"

Mvulana alishangaa kuzungumziwa na Bi Kizee. "Ninakwenda popote. Hakuna yeyote anipendaye wala kunizungumzia," alimwambia Bi Kizee.
Bi Kizee alimwuliza ikiwa angehitaji usaidizi. "Ndiyo," alijibu haraka.

Bi Kizee alimwambia, "Kabla sijakusaidia, nataka ulambe uso wangu hadi upendeze."
Mvulana alikubali kuulamba uso wa Bi Kizee yule ili asaidiwe.

Aliulamba uso wa Bi Kizee kuanzia machoni, akamfuta kamasi puani na kumtoa nta masikioni. Aliulamba uso wa Bi Kizee hadi ukapendeza.
Uso wa Bi Kizee ulimetameta na akamshukuru.

Alisema, "Humu msituni utapata vitu vingi vya ajabu, lakini usichukuwe chochote ila tu mzizi utakaoupata."
Mvulana alitamani sana kuviona vitu vyote vya ajabu. Kabla hajaingia msituni, Bi Kizee alimwita, "Hebu, rudi hapa!" "Niko hapa!" mvulana alisema.

Bi Kizee alimwuliza, "Ulisikia nilichosema? Msituni, utapata vitu vingi vya ajabu, lakini usichukuwe chochote ila tu mzizi utakaoupata." 
Mvulana aliitikia na akakubaliwa kuingia msituni.
Alipoanza kukimbia kwenda msituni, alisikia sauti, "Wewe, rudi hapa!" mvulana hakujua alichotaka yule Bi Kizee. Akarudi.

Bi Kizee alimwambia, "Sina hakika kama umenielewa. Nimesema, utapata vitu vingi vya ajabau msituni, lakini usichukuwe chochote ila mzizi utakaoupata." Mvulana aliitikia na kisha akakimbilia msituni.
Mara tu alipoingia msituni, aliisikia sauti ya Bi Kizee tena, "Rudi hapa!" mvulana alijaribu kuipuuza, lakini sauti ikaendelea kumwita.

Bi Kizee akasema, "Sina uhakika utatenda ninavyokwambia. Utapata vitu vingi vya ajabu msituni, lakini usichukuwe chochote ila tu mzizi utakaoupata." Mvulana alianza kuudhika na marudio haya. Alikimbia hadi msituni.
Mle msituni, aliliona bakuli lililojaa fedha tele. Alizichukuwa na kuziweka mfukoni.

Mara akakumbuka alichoambiwa na Bi Kizee.

Polepole, alizitoa fedha mfukoni na kuzirejesha kwenye bakuli.
Kisha akatazama karibu naye akaona nguo mpya nzuri. Akavua nguo alizokuwa nazo na kuvaa zile mpya.

Halafu akakumbuka aliyoambiwa na Bi Kizee.

Haraka, akazivua zile nguo mpya na kuvaa alizokuwa nazo.
Alipotazama hapo kando, aliuona mzizi! Ulikuwa umenyauka kutokana na jua.

Akajiuliza, "Bi Kizee atafaidikaje na mzizi huu?"

Juu ya mzizi, kulikuwa na bakuli la chakula kilichonukia. Mvulana akahisi njaa. Hakuweza kujizuia kukila.
Ghafla, akakumbuka alichoambiwa na yule Bi Kizee!

Alikumbuka aliambiwa auchukuwe mzizi tu.

Alianza kuutafuta mzizi, lakini hakuupata.
Akiwa ameudhika, alirudi kumwambia yule Bi Kizee kilichotokea. 

Bi Kizee tayari alikuwa ameenda zake.
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mvulana aliyechukiwa na wote
Author - Phumy Zikode
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs
© African Storybook Initiative 2015
Creative Commons: Attribution 4.0
Source www.africanstorybook.org
Menu
  • Navigate

    Navigate through the story by swiping right or left or clicking when the cursors changes to an arrow on the right or the left edge of the screen.

    Tap or click on the centre of the page to see, or remove the menu bars at the top and the bottom of the screen. You can also use the ESC key.

    You can use the slider at the bottom as a way to move quickly through the story. On a mobile device tap on the slider before you drag the slider button.

    Click or tap to return to African Storybook.

  • Share
    If you have a Twitter or Facebook account, you can share this story on your page or a page you manage. You can also copy the web link (URL) for this story.
    • Twitter
    • Facebook
    • Url
  • Rate
    Other visitors rated this story

    Tell us how much you liked the story – drag the scroller to highlight one or more stars
    • Submit
  • Comment
    Read other people’s comments on the story, or add your own.
    • Enter your comment
    • Name
    • E-mail
    • Post
  • Translations and adaptations
    • Musankwa watakali kuyandwa amuntu
      ChiTonga (Translation)
    • Munyamata wamene sanali kukondedwa
      CiNyanja (Translation)
    • The boy who nobody loved
      English (Translation)
    • Picture story 15
      English (Adaptation)
    • Le Garçon Que Personne N’Aimait
      French (Translation)
    • Umulumendo Uo Abantu Baashatemenwe
      IciBemba (Translation)
    • Inkwenkwana eyayingathandwa mntu
      isiXhosa (Translation)
    • Umfana owayengathandwa muntu
      isiZulu (Original)
    • Umusooleli abe isi buli muundu akhakana ta
      Lumasaaba (Translation)
    • Edia Lope Aminae
      Ng’aturkana (Translation)
    • Omusiani Owa Buli Omundu Yaloba
      Oluwanga (Translation)
    • O Menino De Que Ninguém Gostava
      Portuguese (Translation)
    • Mosimane yo o neng a sa ratiwe ke batho
      Setswana (Translation)
    • Mushimani Yanasalatwi Ki Mutu
      SiLozi (Translation)
    • El niño al que nadie amaba
      Spanish (Translation)
  • Download to read
    Landscape version
  • Download to print
    Portrait (booklet) version
  • Download EPUB