Kalabushe, Chiriku
Gaspah Juma
Jesse Breytenbach

Hapo kale, kuliishi msichana aliyeitwa Kalabushe.

Kalabushe alikuwa chiriku.

Alionywa na mamake kutozungumza sana, lakini hakusikia.

1

Siku moja, shangaziye Kalabushe aliugua.

Aliishi ng'ambo mbali kidogo nao.

2

Mamake Kalabushe alikuwa na shughuli nyingi siku hiyo.

Kalabushe alipopewa chakula kumpelekea shangaziye, tayari ilikuwa jioni.

3

Njiani, Kalabushe alikutana na Sinisou.

Sinisou alikuwa fisi aliyegeuka mtu.

4

Sinisou alimwuliza alichobeba. Kalabushe alijibu, "Nimebeba nyama, mayai na maziwa."

Kalabushe alikuwa ameonywa kutotambua alichokuwa amebeba.

5

Kalabushe vilevile alimwambia Sinisou kuwa shangaziye alikuwa mgonjwa na kwamba alikuwa anampelekea chakula hicho.

Sinisou alidondokwa mate alipofikiria juu ya nyama aliyoibeba Kalabushe.

6

Sinisou alikimbia mbele haraka haraka.

Aliingia nyumbani kwa shangaziye Kalabushe.

7

Sinisou alimmeza shangazi.

Alijigubika blanketi lake akasubiri Kalabushe afike.

8

Kalabushe alipowasili, nyumba ilikuwa kimya kabisa.

Aliingia ndani na kuita, "Shangazi, uko wapi? Nimekuletea chakula ule."

9

Kalabushe hakumsikia shangaziye.

Aliingia ndani ya chumba ambamo kawaida shangaziye alilala.

Alishangaa alimpomwona mtu amejigubika blanketi.

10

"Shangazi, mbona masikio yako ni makubwa sana leo?" Kalabushe aliuliza.

Sinisou alijibu kutoka ndani ya lile blanketi kubwa, "Ili niweze kukusikia vyema."

11

Kalabushe aliuliza tena, "Shangazi, mbona macho yako ni makubwa sana leo?"

Sinisou alijibu, "Ili niweze kukuona vyema."

12

Mwishowe, Kalabushe aliuliza, "Shangazi, mbona mdomo wako ni mkubwa sana leo?"

Sinisou alijibu, "Ili niweze kukumeza."

Kisha Sinisou aliruka na kummeza Kalabushe.

13

Kawaida, Kalabushe alipenda kuongea sana.

Alizidi kuzungumza na kuuliza maswali mengi hata alipokuwa mle tumboni kwa Sinisou.

14

Hatimaye, Sinisou alichoshwa na maswali mengi aliyouliza Kalabushe.

Akaamua kumtema nje.

15

Kalabushe na shangaziye waliokolewa na wanakijiji.

Tokea siku ile, Kalabushe alikoma kuzungumza sana hasa, na watu asiowajua.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Kalabushe, Chiriku
Author - Gaspah Juma
Illustration - Jesse Breytenbach
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs