Mamba na Nyani
Basilio Gimo
Jeremiah Dube

Nyani na Mamba walikuwa marafiki wa dhati.

Walicheza pamoja. Walikula pamoja. Walifanya kila kitu pamoja.

1

Siku moja, Mamba alikuwa mgonjwa mahututi. Alikuwa karibu kufa.

Mamba alienda kwa mkanga. "Kama unataka kupata nafuu, itakubidi ule nyama ya Nyani," mkanga akamwambia.

2

Aliposikia haya, Mamba alilia.

Kama angetaka kupata nafuu, hakuwa na jingine ila kumla rafikiye, Nyani.

3

Nyani alipoenda kumwona rafiki yake Mamba, aliupanda mgongo wake.

Mamba alimpeleka Nyani mtoni kwenye maji mengi.

4

"Ni nini kinachokutatiza, rafiki yangu?" Nyani aliuliza.

Mamba alisema, ''Mkanga aliniambia kuwa kama ninataka kupata nafuu lazima nikule wewe, rafiki yangu."

5

Nyani akajibu, "La hasha! Huwezi kunila. Mimi ni mdogo mno!

Subiri nimwite babu yangu. Ni mkubwa kuniliko mimi. Ukimla yeye utashiba."

6

Mamba akauliza, "Yu wapi huyu babu yako?"

Nyani akajibu, "Yuko mtini kule kisiwani."

Mamba akasema, "Nenda ukamlete ili nimle."

7

Nyani aliruka na kukimbia moja kwa moja hadi mtini.

Mamba akangoja na kungoja lakini Nyani hakurudi.

Na huo ndio ukawa mwisho wa urafiki wao.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mamba na Nyani
Author - Basilio Gimo
Translation - Geraldine Nanjala
Illustration - Jeremiah Dube, Little Zebra Books
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs