Mke-mwenza mwenye wivu
Mary Narebon
Jacob Kono

Hapo kale kulikuwa na wake wenza wawili. Waliishi katika nyumba moja na mume wao.

1

Kwa muda mrefu hakuna mke aliyejaliwa kupata watoto. Hatimaye, mke wa kwanza alishika mimba.

Alipojifungua mtoto, mume wao hakuwa nyumbani.

2

Mke wa pili aliwaonea wivu mke wa kwanza na mtoto wake.

Alianza kuwaza jinsi atakavyomwua mke mwenziwe ili awe mke wa pekee.

3

Nyakati hizo, watu hawakuzoea kupika chakula.

Walivila vyakula vikiwa vibichi.

4

Mke wa pili alisema, "Nitakipika chakula ili nimdhuru mke-mwenzangu."

Yeye aliamini kuwa chakula kilichopikwa kingeweza kumwua mtu.

5

Basi alianza kumpikia mke mwenziwe chakula.

Lakini, badala ya kufa, mke wa kwanza alizidi kuwa na afya nzuri kwa sababu ya kula chakula kilichopikwa.

6

Mume wao aliporudi nyumbani, alimkuta mtoto mchanga na mke wa kwanza mwenye afya. Pia alitambua kuwa chakula kilikuwa kikipikwa.

7

Mume huyo alishangazwa na upikaji wa chakula. Akauliza, "Nani aliwafunza kupika chakula?"

Mke wa pili akamnong'onezea mumewe, "Ninakipika chakula ili nimue mke mwenzangu."

8

"Ninamwonea wivu kwa sababu alimpata mtoto ilhali mimi sina. Nina wasiwasi kuwa utanifukuza ubaki naye."

9

Mumewe alikasirika kisha akamuonya, "Acha kuwa na fikira hizo mbaya."

10

Kisha yule mume aliwaleta wakeze pamoja.

Aliwapatanisha wakaishi kwa amani.

11

Walikubali kuendelea kupika chakula kwa sababu kiliwafanya kuwa na afya nzuri.  

Na hivi ndivyo upikaji wa chakula ulivyoanza!

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mke-mwenza mwenye wivu
Author - Mary Narebon
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Jacob Kono
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs