Utata baina ya kazi tofauti
Beatrice Inzikuru
Wiehan de Jager

Katika kijiji kimoja, watu walitofautiana kuhusu kazi gani iliyo muhimu.

Kila mmoja aliamini kuwa kazi yake ndiyo iliyokuwa muhimu zaidi!

1

Mwalimu alisema kazi yake ndiyo iliyokuwa muhimu zaidi.

"Bila walimu, hakuna yeyote atakayeweza kwenda shule kujifunza."

2

Mjenzi akasema kwamba kazi yake ndiyo iliyokuwa muhimu zaidi.

"Bila wajenzi, hakungekuwa na shule za kusomea wala nyumba za kulala."

3

Seremala naye akasema kwamba yeye ndiye aliyekuwa na kazi muhimu zaidi.

"Bila maseremala, hakungekuwa na samani
za kutumia nyumbani na shuleni."

4

Daktari naye alidai kuwa alikuwa na kazi iliyo muhimu kuliko zote.

"Bila madaktari na wauguzi, watu wangeugua na kufa."

5

Mkulima akasema kwamba kazi yake ni muhimu zaidi.

"Bila wakulima, hakungekuwa na chakula."

6

Mwanafunzi naye alisema kuwa wanafunzi ndio walio na kazi muhimu kwa zote.

"Bila wanafunzi, hakungekuwa na walimu, wajenzi, madaktari, wakulima, wala maseremala."

7

Hatimaye, kila mmoja alikubali kwamba
kazi zote ni muhimu. Tunahitaji walimu, wajenzi, madaktari, wakulima, na maseremala.

Lakini, lazima kila mmoja awe mwanafunzi kwanza!

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Utata baina ya kazi tofauti
Author - Beatrice Inzikuru
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs