Nyani aliyekuwa chifu
Bonsamo Miesso
Isaac Okwir

Don alikuwa nyani mkubwa. 

Alikuwa mchokozi.

1

Don ndiye alikuwa chifu wa nyani wengine.

2

Wafuasi wake walimpatia kitambaa maalum.

3

"Nitakivaa kichwani," Don alisema.

4

"Kila mmoja afuate masharti yangu. Msinihoji!"
Don alipiga kelele.

5

Wafuasi walimfuata chifu wao.

Don iliporuka, kila mmoja aliruka.

6

Lakini, kile kitambaa, kilimkaza sana.

7

Don aligusa kichwa alikoumia.

Nyani pia waligusa vichwa vyao.

8

"Hapa panuma," Don alisema.

Nyani pia walisema, "Hapa panauma."

9

Alisema, "Hii imekazika sana!"

Wao pia walisema, "Hii imekazika sana."

10

Don alianguka kutoka juu.

Wote walimuiga wakaanguka.

11

Nyani aliyekuwa chifu alikufa.

Wafuasi wake waliumia, lakini waliishi.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Nyani aliyekuwa chifu
Author - Bonsamo Miesso, Elizabeth Laird
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Isaac Okwir
Language - Kiswahili
Level - First words