Ushauri mbaya
Magabi Eynew Gessesse
Brian Wambi

Kombe na Juma walikuwa maskini pia jirani.

Walifanya kila kitu wenyewe.

1

Walitamani kuwa na punda.

Punda angewabebea mizigo.

2

Kombe akasema, "Hebu tununue punda pamoja."

Walifurahia hatua hiyo.

3

Babake Kombe alipofariki, Kombe alitajirika.

Alimsahau Juma.

4

Kombe alitaka nyama ya punda amlishe mbwa wake.

Juma alihitaji punda.

5

Hakimu aliwaambia, "Kila mmoja wenu anaweza kuchukua nusu ya punda."

6

Kombe alimchinja punda.

Juma alijibebebea vitu kwa mara nyingine.

7

Kombe alitaka kuteketeza chumba chake ili ajenga kipya.

8

Juma alisema, "Changu pia kitachomeka."

Hakimu alikubaliana na Kombe.

9

Chumba cha Juma kiliungua.

Hakimu alisema, "Kombe aliteketeza chake."

10

Juma hakuwa na punda wala chumba.

Alilala chini ya mti.

11

Juma alifanya kazi kwa bidii.

Alipata mazao mazuri ya mbaazi.

12

Wavulana wa Kombe walikula mbaazi karibu wazimalize zote.

13

Walimwambia Juma, "Nenda umwulize baba akulipe mbaazi zako."

14

Juma alisema, "Sitaki pesa zenu. Ninataka mbaazi zangu."

15

Hakimu alimwambia Juma, "Wakate wavulana halafu uchukue mbaazi zako."

16

Juma alikataa kusikiliza alivyoambiwa.

Kombe alilia, "Hebu wazee waamue."

17

Wazee walisema, "Ulimuua punda. Ulichoma chumba chake."

18

Walimwambia Juma, "Kuwaua wavulana wa Kombe ni vibaya pia."

19

Kombe alimpatia Juma nusu ya mali yake.

Wakaishi kwa furaha.

20
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Ushauri mbaya
Author - Magabi Eynew Gessesse, Elizabeth Laird
Translation - African Storybook
Illustration - Brian Wambi
Language - Kiswahili
Level - First words