Chungu kilichokufa
Peter Kisakye
Emily Berg

Biantaka alikuwa na ng'ombe.

Alikuwa pia na chungu kidogo cha maji.

1

Alienda kwa jirani yake kuomba chungu kikubwa.

2

Biantaka aliweka chungu kidogo ndani ya kile kikubwa.

3

Alivibeba vyungu vyote akampelekea jirani yake.

4

Biantaka alimwambia jirani, "Chungu chako kilizaa."

5

Biantaka alirudi kwa jirani kuomba chungu tena.

6

Hakukirejesha.

Jirani aliamua kwenda kumwuliza.

7

Biantaka alisema, "Kilikufa. Nilikuwa najitayarisha kuja kukwambia."

8

Jirani alipiga kelele, "Sijawahi kusikia chungu kikifa!"

9

Biantaka alijibu, "Rafiki yangu, kila kitu kinachozaa lazima kife."

10

Jirani alienda mahakamani kumshtaki Biantaka.

11

Hakimu alisema, "Kila kiumbe hai kinachozaa, lazima kife."

12

Biantaka alipata chungu kikubwa.

Jirani yake akakipoteza chungu chake.

13
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Chungu kilichokufa
Author - Peter Kisakye
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Emily Berg
Language - Kiswahili
Level - First words