Hapo zamani, Sungura na Fisi walikuwa marafiki wazuri.
Sungura alimwambia Fisi, "Ningependa tulime pamoja."
Sungura alionelea wapande mahindi na wagawane majukumu.
Sungura alimwambia Fisi, "Kazi yangu ya kuwafukuza ndege ni ngumu."
Fisi alikubali kulima shamba peke yake.
Wakati Fisi aling'oa magugu, Sungura aliketi chini akiimba.
Mahinid yalipokuwa tayari, Sungura alifurahi kuwafukuza ndege.
Sungura alisema, "Nitavuna yaliyo juu ya udongo. Utavuna yaliyo chini."
Sungura alivuna mahindi yote akahifadhi.
Fisi alikuta mizizi tupu chini ya udongo.
Fisi aligundua kwamba alikuwa amedanganywa. Alikasirika sana.
Walipanda viazi. Fisi alisema, "Nitavuna yaliyo juu ya udongo."
Walifanya kazi pamoja shambani wakiimba.
Wakati wa kuvuna, Fisi alivuna majani ya viazi pekee.
Sungura alivuna viazi vingi vikubwa akahifadhi.
Fisi alimkimbiza Sungura akitaka kulipiza kisasi. Urafiki wao uliisha.