Simba Jike na Mbuni
Daniel Nanok
Brian Wambi

Mbuni na Simba Jike walikuwa marafiki wakati mmoja.

1

Mbuni aliwalisha wanawe vyema.

Walikuwa wenye afya nzuri.

2

Watoto wa Simba Jike walikonda.

Hawakupata chakula cha kutosha.

3

Simba Jike alitamani vifaranga wa Mbuni kuwa wake.

4

Siku moja, Mbuni alikwenda safari.

Simba Jike alichukuwa vifaranga wake.

5

Mbuni aliporudi, aliuliza, "Watoto wangu wako wapi?"

6

Mbuni alimkuta Simba Jike na watoto wake.

7

Simba Jike alimwambia, "Vifaranga ni wangu sasa. Wachukue wana simba."

8

Mbuni alijiuliza, "Nitawapataje wanangu?"

9

Mbuni aliitisha mkutana wa wanyama wote.

10

Wanyama walifika kuhudhuria mkutano.

11

Tembo aliwauliza Mbuni na Simba Jike kujieleza.

12

Wanyama wengi waliogopa kumulaumu Simba Jike.

13

Kichakuro alisema, "Watoto wanaofanana na ndege, ni wa Mbuni."

14

Baada ya kusema hivyo, Kichakuro alitoroka akaingia shimoni.

15

Simba Jike alikasirika sana.

Alirudi kwake na wana simba.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Simba Jike na Mbuni
Author - Daniel Nanok
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Brian Wambi
Language - Kiswahili
Level - First words