Anansi mvivu
Ghanaian folktale
Wiehan de Jager

Anansi ni buibui mvivu.

1

Anapenda chakula, lakini hapiki kwani ni mvivu.

2

Anansi anamtembelea Sungura.

Anaomba wale mboga pamoja.

3

"Nisaidie kukoroga," Sungura anasema.

Anansi hataki, ni mvivu.

4

"Nitarudi baadaye," Anansi anasema.

5

Anafunga utando mguuni na kwenye chungu cha Sungura.

6

"Vuta utando mboga zitakapoiva," Anansi anasema.

7

"Kima, naomba nile maharage nanyi?"

"Tusaidie kufanya kazi."

8

"Nitarudi," Anansi anasema.

Anafunga utando zaidi.

9

"Ngiri, tule viazi pamoja?"

"Nisaidie kuvitayarisha," Ngiri anamjibu.

10

"Nitarudi," Anansi anasema.

Anafunga utando zaidi.

11

Hatimaye, kila mguu wa Anansi umefungwa kwenye chungu.

12

Anansi anavutwa kwenye mguu wa 2.

Halafu mguu wa 3.

13

Miguu yote 8 inavutwa!

"Acheni kuvuta!" Anansi analia.

14

Hakuna anayemsikia Anansi.

Utando unakatika mmoja mmoja.

15

Ndiyo sababu buibui wote wana miguu mirefu myembamba.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Anansi mvivu
Author - Ghanaian folktale
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - First words