Fisi, Sungura na Beseni
Charles Katiwa Kiema
Salim Kasamba

Fisi na Sungura walikuwa marafiki.

1

Sungura alikuwa na punda wake.

Alikuwa pia na beseni ndogo nyekundu.

2

Sungura alimwomba Fisi beseni yake kubwa ya bluu.

3

Fisi alihitaji beseni yake ili afue nguo zake.

4

Fisi alisema, “Ninahitaji beseni yangu kubwa.”

5

“Beseni yako ilizaa mtoto.” Fisi alibeba beseni mbili.

6

Siku nyingine, Sungura aliomba tena beseni ya Fisi.

7

Fisi alipoendea beseni yake, alipata ujumbe mbaya.

8

"Beseni yako ilifariki."  Fisi hakuweza kuamini hili.

9

Fisi aliwaita wanyama wakubwa waamue ukweli.

10

"Viumbe vilivyo hai na vinavyozaa, pia hufa," Sungura alisema.

11

Wanyama walikubali. Fisi aliipoteza beseni yake.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Fisi, Sungura na Beseni
Author - Charles Katiwa Kiema
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Salim Kasamba
Language - Kiswahili
Level - First words