Mbuni na Simba
Daniel Nanok
Brian Wambi

Mbuni na Simba walikuwa marafiki sana.

Kila mmoja alikuwa na watoto wachanga.

1

Mbuni aliwalisha watoto wake vizuri.

2

Watoto wa Simba hawakupata chakula cha kutosha.

3

Simba aliwaangalia vifaranga na kuwaza, "Hawa ni wazuri! Natamani wangekuwa wangu!"

4

Wakati Mbuni alikuwa hayupo, Simba aliwachukua watoto wa Mbuni akaenda nao nyumbani kwake.

5

Mbuni alirudi na kupata watoto wa Simba nyumbani kwake.

Alifadhaika na kujiuliza, "Watoto wangu wako wapi?"

6

Mbuni alikimbia nyumbani kwa Simba.

Aliwapata wanawe wakiwa na Simba.

7

Simba alikataa kuwarudisha watoto wa Mbuni.

Alisema, "Hawa ni wangu sasa. Unaweza kuwachukua wangu."

8

Mbuni alikasirika sana.

"Nitafanyaje ili niwapate watoto wangu?" alijiwazia.

9

Halafu alifikiri, "Ninajua nitakachokifanya. Nitawaita wanyama wote kwa mkutano."

10

Wanyama walikubali kukutana.

11

Tembo aliwauliza Mbuni na Simba kuzungumza.

12

Wanyama wengi waliogopa kumlaumu Simba.

13

Mwishowe, Kichakuro alisimama na kusema, "Watoto ambao wanafanana na ndege ni wa Mbuni. Watoto ambao wana mikia ni wa Simba."

14

Kichakuro alitorokea tunduni.

Wanyama wote walishangilia.

15

Simba alikasirika sana.

Alienda nyumbani na watoto wake.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mbuni na Simba
Author - Daniel Nanok
Translation - Susan Kavaya
Illustration - Brian Wambi
Language - Kiswahili
Level - First sentences