Kima na kiangazi
Alice Edui
Salim Kasamba

Hapo kale kiangazi kilienea nchi nzima. Miti ilisinyaa. Mito ilikauka.

Watu na mifugo wakakosa maji na chakula. Walikonda sana.

1

Kima wengi walioishi milimani walikufa kwa njaa.

Siku moja, Kima mmoja wa kike alitaka kutafuta suluhu. Alienda kutafuta sehemu isiyo na kiangazi.

2

Alisafiri kwa siku nyingi.

Alipita vichaka, akapanda milima na kuvuka mabonde.

3

Hatimaye, Kima huyo alifika mahali palipoitwa Tirkol.

4

Alipata matunda aina nyingi na mto uliobubujika maji.

Alifurahi sana.

5

Kima yule alipiga kambi hapo. Alikula matunda mengi. Akanona na kumetameta.

Kwa furaha, aliogelea mtoni kila siku.

6

Baada ya muda, aliamua kurudi milimani. Alitaka kujua walionusurika na athari za kiangazi.

Alibeba matunda mengi akipitia njia aliyoitumia awali.

7

Alipofika milimani, kima walionusurika walimlaki.

8

Kila mmoja wao aliyataka yale matunda aliyoyaleta.

Walimwuliza, "Ni sehemu gani iliyo nzuri hivi? Tupeleke pia nasi."

9

Kima aliwaelezea uzuri wa Tirkol.

Akakubali kuwapeleka huko.

10

Kima wote walihamia Tirkol.

Walikula matunda, wakanywa maji, wakapumzika na wakanona.

Wakaapa kutorudi milimani tena.

11

Punde, kima wenyeji wa Tirkol waligundua kwamba kima wa milimani walikuwa wamehamia sehemu yao.

12

Walihofia kuwa matunda hayangewatosha.

Wakaamua kuwafukuza kima waliotoka milimani.

13

Siku moja kima wa milimani walikuwa mtoni wakinywa maji.

Kima wa Tirkol waliwavamia kwa mijeledi. Walitaka kuwachapa na kuwafukuza.

14

Kabla ya vita kuanza, kima mmoja mzee aliwauliza, "Mbona mnataka kupigana? Mimi naona kuna chakula cha kututosha sote."

15

Tangu siku hiyo, kima wa kutoka milimani na wale wa Tirkol wamekuwa wakiishi pamoja kwa amani.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Kima na kiangazi
Author - Alice Edui
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Salim Kasamba
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs