Chiriku
Gaspah Juma
Jesse Breytenbach

Chiriku alionywa na mamake kutoongea sana.

Hakutii.

1

Shangazi ya Chiriku aliishi mbali.

Siku moja,alikuwa mgonjwa.

2

Chiriku alitumwa kumpelekea shangazi chakula.

Ilikuwa jioni.

3

Chiriku alikutana na Sinso.

Sinso alikuwa fisi aliyegeuka mtu.

4

Sinso alimwuliza alichobeba.

Chiriku alijibu, "Nimebeba nyama na mayai."

5

Aliongeza, "Ninampelekea shangazi mgonjwa."

Sinso alikitamani chakula.

6

Sinso alimpa kwaheri. 

Alikimbia akajificha nyumbani kwa shangazi.

7

Sinso alimmeza shangazi.

Akajifunika blanketi lake.

8

Chiriku alipowasili, nyumba ilikuwa kimya.

Aliita, "Shangazi, uko wapi?"

9

Hakusikia sauti ya shangazi yake. 

Alishangaa kuona umbo kubwa.

10

Aliuliza, "Mbona una masikio makubwa?"

Sinso alijibu, "Ili nikusikie."

11

Aliuliza tena, "Mbona una macho makubwa?"

Sinso alijibu, "Ili nikuone."

12

Mwisho aliuliza, "Mbona una mdomo mkubwa?"

Sinso alijibu, "Ili nikumeze."

13

Sinso alimmeza Chiriku.

Chiriku aliendelea kuuliza maswali akiwa tumboni.

14

Mwishoni, Sinso alichoka na maswali aliyouliza Chiriku.

Alimtema nje.

15

Chiriku na shangazi yake waliokolewa.

Chiriku alikoma kuongea ovyo.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Chiriku
Author - Gaspah Juma
Adaptation - Ursula Nafula
Illustration - Jesse Breytenbach
Language - Kiswahili
Level - First words