Mayai ya Mamba
Candiru Enzikuru Mary
Rob Owen

Siku moja, Mbwa aliyakuta mayai kando ya mto.

Akajiuliza, "Mayai haya ni ya nani?"

1

Mbwa aliyachukuwa yale mayai na kwenda nayo nyumbani kwake.

2

Alipofika nyumbani, aliyaweka karibu na moto ili yaangue.

3

Mamba alikutana na Mbwa akamwuliza, "Umeyaona mayai yangu?"

Mbwa akamjibu, "La."

4

Mamba akatembea kila mahali akiuliza kila mnyama, "Umeyaona mayai yangu?"

Kila mmoja alimjibu, "La."

5

Mayai yale yaliangua moja baada ya nyingine.

Mamba wachanga walianza kutambaa.

6

Mbwa hakuwalisha wana mamba vizuri.

Walihisi njaa kila wakati.

7

Siku moja, Mamba aliwasikia wanawe wakilia.

Alijua kwamba Mbwa ndiye aliyachukua mayai yake.

8

Alimvamia Mbwa nyumbani kwake akamcharaza kwa mkia.

Mbwa alitorokea dirishani.

9

Mamba alimfukuza Mbwa akitaka kumwadhibu zaidi.

10

Mbwa alimwambia Mamba, "Nisamehe! Sikujua kuwa mayai yalikuwa yako!"

11

Mamba alimsamehe.

Baadaye, aliwapeleka wanawe kuogelea kwa mara ya kwanza.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mayai ya Mamba
Author - Candiru Enzikuru Mary
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Rob Owen
Language - Kiswahili
Level - First sentences