Kwa nini Ajao hakuzikwa
Taiwo Ẹhinẹni
Jesse Breytenbach

Ajao alikuwa popo.

Aliugua nyumbani kwake bila kupata usaidizi wowote.

1

Baada ya muda, Ajao alifariki.

2

Majirani walisema, "Ajao amekufa. Itatubidi tuwaite jamaa zake waje wamzike."

3

Majirani waliwaita ndege wakisema, "Mmoja wenu amefariki. Njooni mkamzike."

4

Ndege walipokuja, waliona kuwa ni Ajao.

Wakasema, "Mnyama huyu si wa jamii yetu."

5

"Wote wa jamii yetu wana manyoya. Lakini Ajao hana manyoya yoyote. Yeye si mmoja wetu."

Kisha ndege hao waliondoka wakaenda zao.

6

Majirani walikubali, "Ndege wamesema ukweli. Ajao hana manyoya. Yeye si wa jamii yao."

7

Kisha mmoja wao akasema, "Labda Ajao ni wa jamii ya panya. Anafanana nao."

8

Majirani waliwaita panya wakisema, "Mmoja wenu amefariki. Njooni mkamzike."

9

Panya walipofika waliona kuwa ni Ajao.

Walisema, "Mnyama huyu si wa jamii yetu."

10

"Kila mmoja wa familia yetu huwa na mkia. Ajao hana mkia."

Kisha Panya waliondoka wakaenda zao.

11

Hakuna jamaa wa Ajao aliyepatikana.

Kwa hivyo, Ajao hakuzikwa.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Kwa nini Ajao hakuzikwa
Author - Taiwo Ẹhinẹni
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Jesse Breytenbach
Language - Kiswahili
Level - First sentences