Mbuzi na kisu cha Fisi
Wekunya Cornelius
Wiehan de Jager

Hapo zamani za kale, kulikuwa na kipindi kirefu cha kiangazi.

Wanyama walikula nyasi zote nchini. Ilisalia tu aina ya mmea uliotambaa kwenye miti mikubwa.

1

Siku moja Mbuzi alimwona Fisi akipita akiwa amebeba kisu.

Mbuzi alikiomba kisu kile ili aukate ule mmea uliotambaa.

2

Fisi alimpatia Mbuzi kisu chake. Mbuzi aliukata mmea ule akaula hadi akashiba kabisa.

Alisahau kisu baada ya kukitumia.

3

Fisi alipokitaka kisu chake, Mbuzi hakujua afanyeje.

Hakuweza kukumbuka alikokitupa.

4

Mbuzi alikwaruza hapa na pale akikitafuta kisu.

5

Fisi alimwambia Mbuzi, "Kwa sababu umekipoteza kisu changu kilichoniwezesha kupata riziki, utakuwa mlo wangu. Vilevile, nitawala wanao."

6

Tangu siku hiyo, Fisi hajamhurumia Mbuzi.

7

Hadi leo, Mbuzi anaendelea kukitafuta kisu cha Fisi.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mbuzi na kisu cha Fisi
Author - Wekunya Cornelius
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Wiehan de Jager
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs