Sungura na Fisi walikuwa marafiki.
Walifanya kazi na kucheza pamoja.
Sungura alisema, "Tulime pamoja."
Fisi akamwuliza, "Tutapanda nini?"
Sungura aliwachunga ndege wasile mahindi.
Fisi alikuwa alime shamba.
Fisi alilalamika.
Sungura akamjibu, "Nitawafukuza ndege wakati wote."
Fisi alikubali kulilima shamba.
Alipomaliza, alipanda mbegu ya mahindi.
Fisi alipalalia mahindi.
Sungura aliketi juu ya jiwe akiimba.
Sungura aliwafukuza ndege kwa furaha.
Hakutoa jasho hata kidogo.
Sungura alisema, "Nitavuna kilicho juu ya udongo. Nawe kilicho chini."
Sungura alitangulia kuyavuna mahindi.
Fisi alikuwa wa mwisho.
Fisi alipata mizizi pekee.
Aliwaza kwa muda mrefu.
Fisi aligundua kuwa Sungura alimdanganya.
Alisema, "Tulime tena pamoja."
Fisi alisema, "Nitavuna vinavyomea juu nawe vinavyomea chini ya udongo."
Wote walilima na kupanda viazi.
Walifanya kazi zote shambani pamoja.
Fisi alienda kuvuna vilivyomea juu ya ardhi.
Alipata majani pekee.
Sungura alivuna viazi vingi.
Fisi alikasirika, "Kwa nini ulinidanganya?"
Fisi alimfukuza Sungura kulipiza kisasi.
Tangu hapo, wakawa maadui.