Paka wa Sigei
Khothatso Ranoosi
Jesse Breytenbach

Sigei anawapenda paka.

Kuna paka wengi nyumbani kwake.

1

Sigei ana paka mmoja mweusi.

Paka huyu anakula nyama nyingi.

2

Sigei vilevile, ana paka mmoja mnono.

Paka huyu hula kila kitu.

3

Paka wa tatu, alipanda mtini na akakwama huko.

4

Sigei alimfuata paka akakwama naye mtini.

Mamake Selemeng alilazimika kumsaidia kushuka chini.

5

Sigei pia ana paka wawili wavivu.

Wanalala nje ya nyumba wakiota jua mchana kutwa.

6

Sigei vilevile, ana paka watatu wanao shughuli nyingi.

Usiku wanawashika panya jikoni.

7

Sigei ana mbwa anayeitwa Lirafi.

Lirafi ana huzuni kwa sababu hana rafiki.

8

Paka wa Sigei hawampendi Lirafi.

Wanapomfukuza, Lirafi anatoroka nyumbani.

9

Sigei anapompata Lirafi, anamrudisha nyumbani.

Paka hawfurahi Lirafi anaporejeshwa.

Hawataki kumwona tena.

10

Sigei ana paka wangapi?

11

Sigei ana mbwa wangapi?

Lirafi yuko wapi sasa?

12

Nyumbani kwenu kuna paka wangapi?

Je, mna mbwa nyumbani kwenu?

13
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Paka wa Sigei
Author - Khothatso Ranoosi, Marion Drew
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Jesse Breytenbach
Language - Kiswahili
Level - First sentences