Binti wa Mflame Kayanja
Amana Yunus
Natalie Propa

Hapo zamani za kale, palikuwa na Mfalme kwa jina Kayanja. Yeye, mkewe malkia na Apenyo binti yao, waliishi katika kasri kubwa.

Apenyo alikuwa msichana mrembo. Kila mwanamume alitaka kumwoa, lakini mfalme Kayanja alitaka mahari ya juu sana.

1

Karibu na kasri la mfalme Kayanja, aliishi Chifu Aludah Mkuu. Aliitwa 'Mkuu' kwa sababu kila aliyeishi pale kijijini, alimtii. 

Chifu Aludah alikuwa amempoteza mkewe kutokana na ugonjwa wa malaria. Alitaka kuoa mke mwingine.

2

Chifu Aludah alikuwa mzee mfupi mwenye upara. Aliamua kupeleka mahari kwa Mfalme Kayanja ili amwoe bintiye.

Walipokuwa wakijadili mahari, Kakembo, kijakazi wa Mfalme, aliyasikia mazungumzo yao.

Kakembo alikuwa na uhusiano wa karibu sana na Apenyo.

3

Chifu Aludah alikubali kumpa Mfalme Kayanja nusu ya mali yake. Pia, alileta sindano ambayo ilikuwa sehemu ya mahari aliyoleta.

Matayarisho ya harusi yalifanywa kisirisiri baina ya Mfalme Kayanja na Chifu Aludah. Mfalme Kayanja alijua kwamba bintiye hangefurahia uamuzi huo.

4

Juma moja kabla ya siku ya harusi hiyo ya kifalme, Kakembo alimjulisha Apenyo.

"Mpendwa binti-mfalme, babako amepanga kukuoza kwa Chifu Aludah. Harusi itafanyika katika muda wa juma moja."

5

Apenyo alishtuka asijue la kufanya. Aliwaza, "Kamwe sitaolewa na yule mzee mwenye upara. Kamwe! Lazima nimwone Trevor, mpenzi wangu. Lazima achukue hatua bila kupoteza muda."

6

Usiku huo Apenyo alitoroka. Babake angegundua alikokuwa akienda angekasirika sana.

Alipitia kwenye msitu wa giza wenye mawe. Mwishowe, akafika kwa Trevor. Aliwasili kwa Trevor akiwa mchovu, mwenye njaa na kiu.

7

Trevor alimkaribisha. "Mpenzi wangu, mbona ukakimbia umbali huu peke yako usiku?" Trevor aliuliza.

Alimletea maji ya kunywa kisha akatulia kumsubiri Apenyo aongee.

8

Apenyo alikunywa maji, akashusha pumzi na kusema, "Babangu anataka kunioza kwa chifu Aludah Mkuu. Lakini, siwezi kuolewa na yule mzee mwovu. Trevor, ningependa kuolewa nawe hata kama wewe ni maskini. Ninakupenda."

9

"Lakini sina chochote cha kulipia mahari." Trevor alilalama.

Apenyo alijibu, "Naelewa, lakini nataka kuolewa nawe tu."

Apenyo alisema, "Hebu twende kwa Kategga, mwenye mashua, atuvushe hadi upande mwingine wa mto tumuepuke babangu."

10

Mfalme Kayanja alipogundua kuwa bintiye ametoweka, aliamuru msako ufanywe kijijini. Walinzi na askari walimtafuta Apenyo kila mahali, lakini, hawakumpata.

Walirudi na kumwambia Mfalme kwamba Apenyo hakuonekana popote. "Basi tafuteni pia vichakani," Mfalme Kayanja aliamrisha kwa hasira.

11

Trevor na Apenyo walifanya haraka kwenda mtoni.

Wakati huo, mawingu meusi yalianza kukusanyika angani. Dhoruba kubwa ilikuwa inakaribia.

12

Kategga, mwenye mashua, alikuwa anafunga mashua yake Trevor na Apenyo walipofika. Trevor alimwmomba Kategga awavukishe hadi ng'ambo ya pili ya mto.

Kategga alikataa akawaelezea kwamba dhoruba kali ilikuwa inakaribia na ingekuwa hatari kuvuka.

13

Trevor alisizitiza huku akimwelezea kwa nini itawalazimu kuvuka  wakati huo. Alitia mkono mfukoni na kutoa kete yenye thamani na kumpa Kategga.

Kategga aliwaonea huruma akakubali kuwavusha haraka kabla ya dhoruba.

14

Kategga aliivuta mashua ukingoni. Wakaabiri na kuanza safari.

Mfalme Kayanja na Chifu Aludah walipofika ufukweni, waliwaona watu watatu mashuani wakivuka.

Wakatambua kwamba Apenyo alikuwa anatoroka.

15

Dhoruba kali ilisababisha mawimbi makubwa. Kategga alishindwa kudhibiti mashua.

Mfalme alilia, "Tafadhali rudini! Nawasamehe." Mayowe yake yalikuwa ya bure. Mashua ilipinduka wote wakazama.

Tangu siku hiyo, walioishi katika ufalme wa Kayanja, walimwoa waliyemtaka, tajiri au maskini.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Binti wa Mflame Kayanja
Author - Amana Yunus
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Natalie Propa
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs