Kima ala mkia wake
Mozambican folktale
Horácio José Cossa

Hapo zamani za kale, Sungura alikuwa rafiki mkubwa wa Kima mwenye rangi ya kijani kibichi.

1

Siku moja Sungura alisema, "Hebu twende matembezi tukatafute chakula." Kima alikubali, lakini ulikuwa mtego kwake!

2

Walienda katika shamba la mahindi na kuanza kula.

3

Sungura mwakili alikuwa amezungumza na mwenye shamba.

Alitaka Kima ashikwe kuonyesha kuwa alikuwa mjinga.

4

Sungura mwakili alianza kupiga kelele, "Wezi! Wezi! Mahindi yako yameisha yote!"

Kisha akaruka, akatoroka na kwenda zake.

5

Ghafla, wenyewe walifika na kumpata Kima akijaribu kutoroka.

Kwa vile alikuwa na mkia mrefu, hakuweza kwenda kwa kasi.

6

Wenyewe walimfuata wakipiga kelele, "Simama! Simama! Tulikuona, wewe ni yule Kima mwizi."

7

Walimshika na kuanza kumpiga.

8

Hakuweza kustahimili uchungu kwa hivyo alisema, "Nilikuwa na rafiki yangu Sungura. Ni yeye aliyenialika."

9

Hata hivyo, wenyewe waliukata mkia wake na kumwambia, "Nenda kamwambie rafiki yako kuwa tuliukata mkia wako!"

10

Walipoondoka, Sungura alinyemelea na kuuchukua mkia wa Kima na kuupika.

Kisha Sungura alimualika kima kwa chakula cha mchana.

11

Mwisho wa mlo Sungura alimwuliza Kima ikiwa alijua alichokula.

Kima mjinga alijibu, "La, sijui!"

12

Sungura alimwambia kuwa alikuwa amekula mkia wake mwenyewe kisha akatoroka.

Kutoka siku hiyo, walikuwa maadui!

13
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Kima ala mkia wake
Author - Mozambican folktale
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Horácio José Cossa
Language - Kiswahili
Level - First sentences