

Nala na Naka wako katika kambi iliyopangwa na shule.
Wanaweka hema zao kisha wanatazama machweo ya jua.
"Inapendeza," Nala anashusha pumzi kwa furaha.
Wanatazama jua likizama chini ya upeo wa macho upande wa magharibi.
"Kuna mwezi kamili usiku wa leo," Naka anatambua hili mwezi unapochomoza upande wa mashariki.
Watoto hao wanalala chali na kusoma anga la usiku.
Naka anashangaa, "Kuna nyota nyingi, na zinang'aa kama almasi!"
Naka anasema, "Mwezi unang'aa kwa sababu unaakisi mwanga wa jua.
Wakati mwezi ni kamili, inaonekana kama mwezi mzima unawaka."
Nala anakubali, "Mwezi huzunguka dunia.
Mara nyingine tunaweza kuona sehemu tu ya mwezi imeangaza, na inaonekana kama ndizi."
Nala anaendelea, "Mwezi unaonekana kama mpira wa miguu wakati wa mwezi kamili.
Mwezi unaposonga, tunaona nusu ya mwezi. Unaonekana kama ndizi."
Naka anasema kwa maringo, "Nilijua hilo!
Nilijua pia kuwa mwezi huzunguka dunia na pamoja vyote huzunguka jua."
Nala anatabasamu, "Je, ulijua kwamba jua ni nyota?"
Anaongezea, "Jua ni nyota kubwa ya gesi zinazowaka, zikizalisha mwanga na joto."
Naka anatambua, "Bila taa za mji, tunaona anga ya usiku kwa uwazi.
Anga za juu huanzia juu ya safu ya hewa karibu na dunia, lakini anga za juu huishia wapi?"
Nala anatabasamu, "Tutakuwa wanaaga na kusafiria chombo cha anga chenye kasi zaidi.
Tutapita sayari na nyota za mbali zaidi. Halafu tutajua anga za juu zinaishia wapi."
Maswali
1. Hadithi inawahusu nani? Wanafanya nini?
2. Mwezi kamili ni nini? Uchore.
3. Mwezi huchomozea wapi?
4. Ni nyota ipi iliyo karibu na dunia?
5. Kuna sayari 8. Tafuta majina yake.
6. Chora picha ya jua na sayari.


