Naka na Nala wanaongea kuhusu hewa
Ndivhuho Mutsila
Simon Mokoena

Naka na Nala wako katika uwanja mkavu, wakiwa wameketi chini ya mti.

Nala anaskia majani yakipepesuka kutokana na upepo mwanana.

1

"Sikiliza Naka, unaweza kusikia sauti ya majani?" Nala anauliza.

"Ndiyo, ninaweza kuyasikia na pia kuyaona yakisonga," Naka anajibu.

2

"Je, unakumbuka nini kinachofanya majani kusonga?" Naka anauliza.

"Ni wakati upepo unavuma na kupeperusha vitu," Nala anajibu.

"Ni hewa," Naka anasema.

3

"Hewa inatuzunguka, lakini hatuwezi kuiona," Nala anaanza kusema.

Naka anakatiza, "Lakini tunaweza kuona na kusikia majani yakisonga!"

4

Nala anaendelea, "Hatuwezi kuiona hewa, ila tunaweza kuona na kuskia athari za hewa ikisonga. Huo ni upepo."

"Upepo ni hewa?" Naka auliza.

5

"Ndiyo," Nala anatabasamu.

Anaongeza, "Hewa pia hushikilia matone madogo ya maji kwenye mawingu. Maji hayo yanapozidi kuwa mazito, matone ya maji huanguka kama mvua."

6

"Hebu fikiria ikiwa sisi tunaweza kupaa angani katika puto la hewa moto.

Puto hilo ni kama tone la maji na hewa inalishikilia juu," Nala anasema.

7

"Sisi pia tunavuta hewa," Naka anakumbuka.

"Ndiyo, wanyama wote wnahitaji hewa, hata mimea, ili kuishi," Nala anasema.

"Tunahitaji hewa safi," Naka anakubali.

8

"Hatuwezi kuiona hewa, lakini imeundwa na nini?" Naka anauliza.

"Hewa ni mchanganyiko wa gesi na chembe ndogo za vumbi," Nala anajibu.

9

"Dunia imegubikwa kwa hewa," Nala anasema.

"Hewa iko kila mahali. Hewa ya dunia inatanda kutoka hapa hadi angani," Nala anaongeza.

10

Maswali

1. Hadithi inahusu nani?

2. Wako wapi?

3. Nani ahitaji hewa kuishi?

4. Hewa imeundwa na nini?

5. Hewa iko wapi?

11

6. Mbona matone ya mvua huanguka?

7. Upepo ni nini?

8. Tafuta hadithi kuhu upepo.

9. 'Hewa safi' ni nin?

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Naka na Nala wanaongea kuhusu hewa
Author - Ndivhuho Mutsila
Translation - Anne Kamau
Illustration - Simon Mokoena
Language - Kiswahili
Level - First sentences