Naka na Nala wanaongea kuhusu maji
Eric Khorombi
Simon Mokoena

Naka na Nala wanajifunza kuhusu maji.

"Maji hayana rangi wala ladha, lakini ni rasilimali yenye thamani!" Nala anashangaa.

1

Naka anakubaliana naye, "Watu hutumia maji kunywa, kupika, kusafisha na kulima."

"Na kwa ajili ya kutengeneza vitu viwandani," Nala anaongeza.

2

"Zaidi ya nusu ya mwili wa binadamu imeundwa kwa maji!

Miili yetu inahitaji maji ili kufanya kazi. Viumbe vyote vilivyo hai, vinahitaji maji," Naka anasema.

3

"Sehemu kubwa ya dunia imafunikwa kwa maji kwenye mito, maziwa na bahari," Nala anasema.

Naka aitikia kwa kichwa, "Zaidi ya thuluthi mbili ya sayari yetu ni maji."

4

"Lakini sehemu kubwa ya maji duniani ni maji ya chumvi.

Kiasi kidogo tu ni maji safi ambayo ndio binadamu wanahitaji," Naka anasema.

5

"Maji ya chumvi yana chumvi, na ni ghali kuondoa chumvi kwenye maji.

Lakini, binadamu hawawezi kunywa maji yenye chumvi!" Naka anashangaa.

6

"Kweli, hiyo ndiyo sababu lazima tuchunge vianzo vya maji safi.

Hatustahili kuchafua mito na maziwa kwa uchafu au taka," Nala anasema.

7

"Hebu tujifunze kuhusu mzunguko wa maji.

Ni mchakato unaohusisha maji kutoka ardhini kuelekea angani na kukusanyika kwenye mawingu," Naka anasema.

8

Nala anaongeza, "Maji yaliyo katika mawingu huanguka ardhini kama mvua, mvua ya mawe au theluji."

9

Naka anasema kwa mshangao, "Nina kiu, ninahitaji maji!"

Nala anajibu, "Ndiyo, ubongo wako unahitaji maji ili kufikiria na kujifunza! Maji ni uhai, yatunze vizuri."

10

Maswali

1. Nani anahitaji maji safi? Kwa nini?

2. Orodhesha matumizi 5 ya maji safi.

3. Twanawezaje kutunza maji safi duniani?

11

4. Je, maji mengi ya dunia ni safi au ya chumvi? Eleza.

5. Chora mzunguko wa maji. Tumia maneno kutoka kwenye hadithi kuelezea kinachotendeka.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Naka na Nala wanaongea kuhusu maji
Author - Eric Khorombi
Translation - Anne Kamau
Illustration - Simon Mokoena
Language - Kiswahili
Level - First sentences