Tunaishi katika nyumba ya mviringo
Nina Orange
Vusi Malindi

Watu huishi katika nyumba aina mbalimbali. Baadhi ya nyumba zinajengwa kwa vifaa asilia, kama vile majani au nyasi. Nyumba nyingine zinajengwa kwa vifaa vilivyotengenezwa na binadamu, kama vile kioo na zege.

Baadhi ya nyumba zinajengwa kwa kutumia vifaa vya asilia na vilivyotengenezwa. Mfano ni nyumba ya mviringo inayozungumziwa katika hadithi hii.

1

Kabo na Thabo wanaishi katika Wilaya ya Kgatleng nchini Botswana, karibu na kijiji cha Mochudi. Wanaishi na wazazi wao katika nyumba ya mviringo.

"Nyumba ya mviringo ni aina ya nyumba ya jadi yenye paa la nyasi. Nyumba hizi hujengwa sehemu nyingi za kusini mwa Afrika," Kabo anaeleza.

2

Thabo anaendelea, "Nyingi wa nyumba hizi ni mviringo, na zina mlango na madirisha. Sisi tuna madirisha ya kioo, ambayo hawakuwa nayo zamani."

"Babu yetu alijenga nyumba hii ya mviringo kwa njia ya jadi. Baba yetu aliweka baadhi ya vifaa vya kisasa," Kabo anasema.

3

"Tueleze mchakato wa ujenzi," Kabo anapendekeza.

Anasema, "Wajenzi walitumia mbao, majani makavu, mawe, zege, na plasta.

Walianza kwa kuchimba shimo. Walijaza shimo hilo kwa mawe madogo, udongo, na mchanga. Hii ilifanya msingi kuwa imara na wenye nguvu wa kujenga juu yake."

4

Thabo anaendelea, "Wajenzi walitia miti mirefu ya mbao katika msingi, kuzunguka pembe ya nje. Waliifunga miti pamoja, wakifanya fremu ya mbao kwa ajili ya kuta za nje.

Baada ya muundo msingi kukamilika, wajenzi walitia mawe karibu karibu ndani ya fremu."

5

"Kisha, wajenzi walichanganya udongo, maji, na samadi ya ng'ombe. Hii hufanya zege ya asili ambayo ni ngumu sana inapokauka. Walitia zege kati ya mawe kuyafunga mahali pake," Kabo anasema.

"Kujenga kwa mawe na zege hufanya kuta imara ambazo hudumu kwa muda mrefu," Thabo anaongeza.

6

Kabo anasema, "Kuta kubwa za nje zinazuia joto."

Thabo anaeleza, "Uzibaji huu unamaanisha kwamba ndani kunabaki baridi wakati nje kuna joto jingi. Joto la jua halipenyezi kupitia kuta.

Katika maeneo yenye majira baridi, hii hufanya nyumba ya mviringo kuwa na joto wakati wa majira ya baridi kwa kuhifadhi joto ndani."

7

"Wajenzi waliumba sakafu ya nyumba yetu ya mviringo kwa kujaza udongo katika msingi walioufanya," Thabo anasema.

Kabo anasema, "Kukamilisha sakafu, walieneza safu ya mwisho ya udongo na kuijaza. Hii ilikauka kwa ugumu na kuunda uso uliosawazika, hata kwa sakafu.''

8

Thabo anasema, "Hatua ya mwisho ilikuwa kuweka paa. Nyumba ya mviringo kawaida huwa na paa la majani makavu yenye umbo la ncha.

Wajenzi walifanya fremu ya mbao na miti iliyounganishwa pamoja katika ncha katikati.

Walishonea mafungu ya majani makavu kwenye miti kwa tabaka. Paa la majani makavu ni lenye kuzuia maji."

9

Nyasi ni nyenzo nzuri kwa paa. Lakini nyenzo hii ya asili pia huwa nyumba nzuri kwa wadudu na wanyama wengine. Wengi wao ni wadudu waharibifu!

Angalia picha na utafute: buibui watatu, nge, mende, mchwa, na panya.

10

Vifaa vya asili kama majani makavu ya nyasi hutengeneza mazingira mazuri kwa buibui kuishi na kuwinda.

Buibui hawaharibu paa la majani bali husaidia kudhibiti wadudu wengine.

Tunahitaji kutunza paa la nyasi ili kuwazuia wadudu waharibifu kama panya, viroboto, na mchwa.

11

"Kuna wengi wetu tunaishi katika nyumba kama hii ya mviringo!" anasema Thabo, akitazama paa la nyasi. Anaogopa buibui.

"Ninajiuliza ni wanyama wengine gani wanaoishi karibu nasi?" anauliza Kabo, kwa wasiwasi.

"Nitakapojenga nyumba yangu, nitajenga ya mviringo yenye paa la vigae!" anacheka Kabo.

12
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Tunaishi katika nyumba ya mviringo
Author - Nina Orange, Ursula Nafula
Translation - Anne Kamau
Illustration - Vusi Malindi
Language - Kiswahili
Level - Read aloud