

Siku moja nikiwa nimekaa darasani, nilichungulia dirishani na kuona tai mkubwa wa kahawia akiruka.
Mabawa ya tai yalikuwa wazi lakini hayakupapatika.
Hili lilinifanya niwe na hamu ya kutaka kujua zaidi kuhusu kuruka.
Labda ndege walishawishi uvumbuzi wa chombo cha ndege. Ndege ana mabawa, na ndege, chombo cha kusafiria, pia kina mabawa.
Natamani kuruka, lakini sina mabawa.
Nilienda maktabani kutafuta vitabu kuhusu ndege. Nilitaka kujua jinsi zinavyoruka.
Niliona picha za mashine tofauti za kuruka. Mashine zingine zilikuwa na injini, zingine hazikuwa nazo.
Niliona chombo cha kuning'inia na parachuti.
Niliona roketi, helikopta, zepelini, puto za hewa moto, na ndege za zamani sana. Zile unaweza kupata kwenye sehemu za makumbusho.
Ndege inarukaje? Ndege nyingi za kisasa zinaendeshwa na injini za jeti. Injini za jeti husogeza ndege mbele kwa kasi sana. Hiyo hufanya hewa kutiririka kwa kasi sana juu ya mabawa ya ndege.
Mabawa yanasukuma hewa nyuma kuelekea ardhini. Hiyo husababisha shinikizo la juu au nguvu. Nguvu ya juu inashikilia ndege angani.
Kitu cha karibu zaidi ninachoweza kufanya ili kuruka, ni katika ndege. Umewahi kuwa ndani ya ndege?
Nimekuwa nikitamani kuruka katika ndege kubwa.
Mwalimu wangu alituambia kwamba tunaweza kutimiza matakwa yetu kwa kufunga tu macho na kuwaza juu yake.
Kwenye mawazo yangu, ninasikia:
Mimi ni rubani wako. Mimi ndiye nahodha wa ndege hii.
Tafadhali funga mkanda wa kiti chako na ujiandae kwa safari.
Tayarisha njia ya kurukia ndege, ninaanzisha injini za ndege!
Wewe ni abiria umeketi kwenye kiti cha dirisha.
Tunaenda kwa kasi kwenye njia ya kurukia ya ndege. Tunapaa kutoka uwanja wa ndege.
Injini na mabawa ya ndege zinatusukuma angani. Tutaruka juu zaidi kuliko ndege yeyote.
Mwalimu wangu alisema tunaweza kufanya chochote katika mawazo yetu.
Alisema tunaweza kuwa chochote tunachotaka kuwa, au kufanya chochote tunachotaka katika akili zetu.
Je, ungependa kuruka kwenda wapi?

