Anzani, mwanaanga
Arnold Mushwana
Vidyun Sabhaney

Anzani anaweza kuona kundinyota wakati wa usiku.

Kundinyota ni kundi la nyota linalounda picha au muundo angani. Nyota hizi ziko mbali sana na dunia.

Anzani anataka kuwa mwanaanga atakapokuwa mkubwa. Wanaanga husafiri angani.

1

Hakuna hewa au maji katika anga. Wanaanga lazima wavae suti maalum ili kuishi.

Suti hizo zina oksijeni ya kupumua, na maji ya kunywa.

Suti hizo pia hulinda wanaanga dhidi ya baridi, joto na vumbi la anga.

2

Wanaanga husafiri katika vyombo vya anga, ambavyo ni magari yaliyotengenezwa kuruka angani.

Vyombo vya anga vina injini za roketi zenye nguvu sana.

Injini lazima ziwezeshe chombo kuruka mbali na dunia kabla ya kufika angani.

3

Injini za roketi huchoma mafuta mengi ili kurusha chombo cha anga za juu.

Wakati mafuta yanawaka, husababisha moto nyuma ya roketi.

Nguvu ya mafuta yanayochomeka husukuma roketi kwenda juu. Pia tunatumia roketi kurusha satelaiti angani.

4

Satelaiti nyingi husafiri kuzunguka dunia. Mwezi ni satelaiti ya asili.

Satelaiti zilizotengenezwa na wanadamu hutusaidia kwa shughuli kama vile utabiri wa hali ya hewa na utengenezaji wa ramani.

Satelaiti daima husonga katika mduara kuzunguka kitu kikubwa zaidi angani. Mwendo huu unaitwa obiti.

5

Anzani anajua mengi kuhusu nyota na sayari katika mfumo wetu wa jua na sayari zake.

Anajua majina ya sayari nane zinazozunguka jua.

Anajua kuna nyota moja tu katika mfumo wetu wa jua na sayari zake. Hiyo ni jua.

6

Vimondo pia huzunguka jua. Kimondo ni mwamba wa anga. Vimondo vingi ni chembe za vumbi ndogo, lakini vingine ni vikubwa.

Baada ya kuingia kwenye angahewa inayozunguka dunia, vimondo huanguka haraka na kuchomeka. Vinaonekana kama mipira ya moto au 'nyota risasi'. Mara kwa mara, kimondo huanguka ardhini!

7

Ardhi iko mbali na anga. Darubini inatusaidia kuona vitu vilivyo mbali zaidi kuliko macho yetu yanavyoweza kuona.

Anzani atasoma anga kwa darubini hadi atakapoweza kusafiri angani.

Ili kuwa mwanaanga, unapaswa kupenda masomo ya Sayansi, kama Hisabati, Jiografia, Fizikia, Kemia na hata Biolojia.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Anzani, mwanaanga
Author - Arnold Mushwana, Given J Hlongwani
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Vidyun Sabhaney
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs