

Shika mkono wa mtu mzima au rafiki ukiwa unavuka barabara.
Angalia vizuri pande zote kabla ya kuvuka barabara.
Angalia kulia, angalia kushoto, angalia tena kulia kabla ya kuvuka.
Usikimbie au kucheza barabarani.
Unaweza kugongwa na gari.
Siyo lazima kuongea na watu ambao huwafahamu.
Usiogope kukataa.
Usiogope kukataa maombi yoyote ya mtu ambaye humfahamu.
Vibiriti, vibiriti vya petroli na mishumaa ni vifaa vya watu wazima, siyo vya kuchezea.
Usivichezee, vinaweza kukuunguza.
Usicheze na visu, mikasi au vitu vingine vikali.
Vinaweza kukukata!
Lala ndani ya chandarua ili kujilinda na mbu na magonjwa makali kama malaria.
Kama unahisi una homa na unajisikia kuumwa, nenda hospitali ukapime ili upate dawa sahihi.
Usisogelee maji yenye kina kirefu, mito, maziwa na bahari...
...kama huwezi kuogelea.
Jifunze kuogelea kwa sababu kucheza kwenye maji kunafurahisha kweli.
Usiwasogelee wanyama wakali.
Nyoka wanaweza kuwa na sumu.
Simba, vifaru na nyati wanaweza kukushambulia na kukuumiza.
Kuwa makini ili usiumie.

