

Kwa miezi mingi anga lilikuwa kavu. Lomongin, mbuni mvua maarufu, alizungumza na miungu.
Watu walikusanyika nje ya boma lake. Walingoja kwa hamu na ghamu ujumbe wa matumaini.
Aliwahakikishia watu kwamba muumba angewapa mvua hivi karibuni.
Wangepanda mimea yao.
Watoto walicheza nje tulipokuwa tukingoja mvua.
Baadaye siku hiyo, tuliyaona mawingu meupe mbali mashariki. Nilijua ni mawingu ya mvua.
Watu walikuwa bado wanawaza kuhusu kile mbuni mvua alisema.
Mama alipiga yowe kwa sauti, "Pale! Sasa mawingu ni meusi. Njooni ndani."
Mvua ilinyesha.
Ikanyesha!
Tulikuwa tumeingoja mvua kwa siku nyingi!
Mwanzo, tulifurahi.
Maji yalizidi kuwa kila mahali.
Daraja la kuunganisha kijiji chetu na sehemu nyingine, lilisombwa na maji.
Nyumba zilisombwa na gharika.
Kile kilikuwa baraka, kilikuwa sasa ni mauti kwetu.
Tulikuwa tumejitayarisha kwa upanzi, lakini sasa hatungepanda. Tulikuwa tumeitamani mvua, lakini sasa hatukuitaka tena.
Hatukuwa na daraja la kuvukia. Wengi hawakuwa na makazi wala miji.
Na tulikuwa na shida nyingine! Tuliona mamba wakiogelea kila mahali.
Hili halikuwa limewahi kutokea tena.
Tulichanganyikiwa!
Hatungeenda manunuzi kwa sababu maduka yote yalikuwa ng'ambo ya mto.
Watoto hawangeenda shuleni kwa sababu shule zilikuwa ng'ambo ya mto.
Kile kingekuwa baraka, kiligeuka kuwa laana kwetu. Lomongin, mbuni mvua, akakata tamaa vilevile.
Aliyekuwa na furaha pekee ni Kapuus na paka wake wanane!

