Amara na wanyama
Judy B. Maranga
Sarah Bouwer

Amara alikuwa na umri wa miaka tisa. Alisomea shule ya msingi ya Kerema. Masomo aliyoyaenzi mno ni Kiingereza, Sayansi na Masomo ya Jamii.

Alitaka kuwa wakili atakapokuwa mkubwa. Amara aliwapenda wanyama sana.

1

Amara aliishi na mama yake, Margi. Alikuwa mkulima mwenye bidii.

Baba yake Amara aliaga dunia alipokuwa na umri wa miaka mitano.

2

Wakati Amara hakuwa shuleni, alichukua muda wake kuwa na Mbisi, mbuzi.

Alimsafisha na kumlisha.

3

Amara pia alikuwa na bembeleza wake, Simba. Mama yake hakuwapenda mbwa sana lakini alimruhusu Amara kumweka Simba.

Endapo Simba angemsumbua, angefoka, "Ondoka kabla sijakupiga teke." Amara alihuzunika.

4

Jumamosi moja, walikuwa na wageni kutoka kwa kikundi cha akina mama.

Amara alifurahi kuwa rafiki za mama yake walikuwa wamekuja na watoto wao. Wangecheza kandanda.

5

Mama yake alikuwa ameandaa chakula ambacho kikundi kilipenda.

Amara alikumbushwa na mamaye kumfungia Simba. Aliwabwekea wageni.

6

Amara hakumfungia Simba vizuri. Wageni walishangaa kumwona mbwa chumbani. Mama Oto aliuliza, "Kwa nini mnamruhusu mbwa kuingia ndani ya nyumba?"

Mama alimwita Amara aje amtoe Simba nje.

7

Amara hakusikia mama yake akimwita kwa sababu walikuwa na shughuli za kucheza.

8

Amara alipoenda ndani ya nyumba, alimwita Simba nje. Simba alikuwa mtiifu sana kwa Amara.

Baada ya mlo, wageni walisema, "Tutawatunza pia mbwa wetu vizuri kama Amara. Tunawatesa ilhali wanatusaidia sana."

9

Baadaye, mama alimwomba Amara radhi kwa kuwa mchoyo na katili kwa Simba. Amara alifurahi kwa kuwa mwishowe mama yake alimkubali mbwa wake.

Amara anapokuwa shuleni mama yake humlisha Simba. Rafiki za mama yake wamejifunza kuwa wazuri kwa mbwa wao.

10
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Amara na wanyama
Author - Judy B. Maranga
Translation - Geraldine Nanjala
Illustration - Sarah Bouwer
Language - Kiswahili
Level - Longer paragraphs