Maisha ya viatu
Nozuko Mkizwana
Nozuko Mkizwana

Katika mji fulani, kulikuwa na duka nadhifu la viatu vya bei ghali.

Ni katika mji huu ndimo nilizaliwa.

1

Watu wengi walikuja kwenye duka hilo la viatu, lakini ni wachache tu walioweza kununua viatu hivyo vya mapambo.

Siku moja, mwanamume tajiri mwenye miguu mikubwa alilitembelea duka lile.

2

Aliziweka pesa zake kwenye kaunta.

Kisha, akiwa ameiweka mikono yake mifukoni, alitembea juu na chini akiviangalia viatu.

3

Aliponikaribia, nilikosa pumzi na kuganda.

Aliinyosha mikono yake na kunikamata.

Aliketi na kuanza kunivaa kwenye miguu.

4

Alikuwa na miguu mikubwa, na harufu ilikaribia kunikosesha pumzi!

Nilipakiwa kwenye sanduku.

Tulienda nyumbani, akaniweka kwenye kabati.

5

Alinivaa kila siku.

Nilimfanya akawa nadhifu na akatembea kwa ujasiri.

Nilikuwa na maisha magumu. Kwa kuwa alikuwa mvivu, hakuiosha miguu yake!

6

Kwa upande wangu, nilimng'ata wakati mwingine, na kumfanya achechemee.

Mwishowe, nilizeeka na kuvunjika, nikawa na makovu na nyufa.

Aliniweka nje, karibu na pipa la takataka.

7

Mtu mwingine alinipeleka kwenye karakana ya ngozi ili nichakatwe.

Huko, nilitengenezwa mkoba mpya uliometameta.

Nilianza maisha mapya.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Maisha ya viatu
Author - Nozuko Mkizwana
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Nozuko Mkizwana
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs