

Afifah ni mtoto wa kifaru mweupe.
Walinzi wa wanyama pori walimuokoa kutoka kichakani.
Mama yake aliuawa na majangili.
Walinzi wa wanyama pori walimpeleka Afifah mahali pa usalama.
Afifah aliumia moyoni.
Pia aliogopa kwamba majangili watarudi kuchukua pembe yake.
Polepole, Afifah alipata marafiki.
Alijisikia salama na akacheza matopeni.
Alikunywa maziwa yenye lishe.
Siku moja Afifah alimwuliza rafiki yake Amina, "Kwa nini wanataka pembe zetu?"
Amina akamjibu, "Wanaamini kuwa pembe zetu ni za kimiujiza!"
"Lakini pembe zetu sio za kimiujiza!" Afifah alilia.
"Hapana, bila shaka, sivyo. Pembe ni sawa na nywele na kucha," Amina alisema.
Afifah na Amina ni wa mwisho wa aina yao.
Vifaru weupe wamekaribia kutoweka.
Karibu wote wametoweka kutoka ulimwenguni.
Tunaweza kuwaokoa vifaru weupe na wanyama wengine wanaoelekea kutoweka.
Je, unaweza kufanya nini?
Pata kujua zaidi!

