Yatima
Saajida Patel
Saajida Patel

Afifah ni mtoto wa kifaru mweupe.

Walinzi wa wanyama pori walimuokoa kutoka kichakani.

1

Mama yake aliuawa na majangili.

Walinzi wa wanyama pori walimpeleka Afifah mahali pa usalama.

2

Afifah aliumia moyoni.

Pia aliogopa kwamba majangili watarudi kuchukua pembe yake.

3

Polepole, Afifah alipata marafiki.

Alijisikia salama na akacheza matopeni.

Alikunywa maziwa yenye lishe.

4

Siku moja Afifah alimwuliza rafiki yake Amina, "Kwa nini wanataka pembe zetu?"

Amina akamjibu, "Wanaamini kuwa pembe zetu ni za kimiujiza!"

5

"Lakini pembe zetu sio za kimiujiza!" Afifah alilia.

"Hapana, bila shaka, sivyo. Pembe ni sawa na nywele na kucha," Amina alisema.

6

Afifah na Amina ni wa mwisho wa aina yao.

Vifaru weupe wamekaribia kutoweka.

Karibu wote wametoweka kutoka ulimwenguni.

7

Tunaweza kuwaokoa vifaru weupe na wanyama wengine wanaoelekea kutoweka.

Je, unaweza kufanya nini?

Pata kujua zaidi!

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Yatima
Author - Saajida Patel
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Saajida Patel
Language - Kiswahili
Level - First sentences