Methali za jamii ya Nyungwe
Little Zebra Books
Max Okoto

Kumuua nyani, lazima uwe na macho makavu.

1

Mbwa anayebweka, haumi.

2

Wakati viboko wanapigana, ni nyasi ndizo huteseka.

3

Kifaranga huchafua kiota kwa sababu hivyo ndivyo anaona mamake akifanya.

4

Usiseme kwamba kuna tembo unapokuwa pale juu ya mabega yangu.

5

Chura wote huzaliwa kwa njia ile ile.

6

Kidole kimoja hakiwezi kuua chawa.

7

Simba asiyekuwa na nyama, hula nyasi.

8

Ni mbuzi mdogo aliye nyuma ya kundi ndiye hupatwa na fimbo.

9

Unaogopa giza wakati ambapo hata fisi hawapo.

10

Kinyonga hufa kwa ajili ya aibu.

11

Ili uweze kuyaona macho ya konokono, lazima usubiri.

12

Mchekelee tu kasa, lakini ni yeye ndiye ana maji.

13

Mgeni ndiye humuua nyoka.

14

Fisi anayelilia mashambani hali wimbi.

15

Simba anayekula binadamu haendi nje usiku.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Methali za jamii ya Nyungwe
Author - Little Zebra Books
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Max Okoto
Language - Kiswahili
Level - First sentences