Mbwa wangu wa kupdendeza
Priscilla K
Priscilla K

Mama yangu alinipatia watoto wa mbwa wawili.

Walikuwa maridadi sana!

1

Niliamua kuwaita Kifalme na Jeusi.

2

Kifalme alikuwa wa rangi ya kahawia, na, alikuwa kama malkia.

Jeusi alikuwa mbwa mweusi maridadi mwenye manyoya marefu.

3

Nilizoea kuwatembeza kila siku baada ya kutoka shuleni.

4

Wakati mwingine niliwaosha peke yangu.

Kifalme alipenda kutoroka!

5

Halafu, tulihama na kwenda kwenye ghorofa.

Mbwa hawakuruhusiwa huko.

6

Tuliwaachia binamu zangu Jeusi na Kifalme.

Asubuhi moja, niliamua kuwatembelea mbwa wangu.

7

Nilipata kuwa Jeusi alikuwa amepotea na Kifalme alikuwa mpweke.

Nilihisi vibaya sana moyoni mwangu.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mbwa wangu wa kupdendeza
Author - Priscilla K
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Priscilla K
Language - Kiswahili
Level - First sentences