

Kulikuwa na msichana aliyeitwa Ayanda.
Ayanda alikuwa mtoto wa pekee wa wazazi wake.
Mamake na babake walitaka kutengana.
Ayanda aliamua kutoroka nyumbani.
Alienda msituni kwa sababu hakujua kwingine kwa kwenda.
Mbwa mwitu alimfukuza Ayanda, kwa hivyo alipanda mti.
Mbwa mwitu alijaribu kumuuma, kwa hivyo alipanda juu zaidi.
Akiwa juu ya mti, Ayanda aliliona jua nzuri.
Alilipenda sana jua akaamua kukaa msituni.
Ayanda alipanda mti kila siku kuongea na jua.
Jua likawa familia yake.
Siku moja, Ayanda alimwona mwanamume chini ya mti.
Mwanamume huyo alikuwa babake.
Ayanda alishuka chini na babake akamwelezea kwa nini alikuwa hapo.
Alisema, "Kitambo sana kabla hujazaliwa, mimi na mamako tulikuwa tukikutana hapa. Ni mahali pa pekee. "
"Mimi na mamako tunapogombana, mimi hupanda mti huu ili nipate amani," babake Ayanda alisema.
Baada ya muda mfupi, mamake Ayanda pia alifika pale msituni.
Alikuja kufanya amani na babake Ayanda.
Huu ulikuwa mti wao wenye amani.

