Mti wenye amani
Mpumelelo Mlangeni
Tshiamo Msimanga

Kulikuwa na msichana aliyeitwa Ayanda.

Ayanda alikuwa mtoto wa pekee wa wazazi wake.

Mamake na babake walitaka kutengana.

1

Ayanda aliamua kutoroka nyumbani.

Alienda msituni kwa sababu hakujua kwingine kwa kwenda.

2

Mbwa mwitu alimfukuza Ayanda, kwa hivyo alipanda mti.

Mbwa mwitu alijaribu kumuuma, kwa hivyo alipanda juu zaidi.

3

Akiwa juu ya mti, Ayanda aliliona jua nzuri.

Alilipenda sana jua akaamua kukaa msituni.

4

Ayanda alipanda mti kila siku kuongea na jua.

Jua likawa familia yake.

5

Siku moja, Ayanda alimwona mwanamume chini ya mti.

Mwanamume huyo alikuwa babake.

Ayanda alishuka chini na babake akamwelezea kwa nini alikuwa hapo.

6

Alisema, "Kitambo sana kabla hujazaliwa, mimi na mamako tulikuwa tukikutana hapa. Ni mahali pa pekee. "

"Mimi na mamako tunapogombana, mimi hupanda mti huu ili nipate amani," babake Ayanda alisema.

7

Baada ya muda mfupi, mamake Ayanda pia alifika pale msituni.

Alikuja kufanya amani na babake Ayanda.

Huu ulikuwa mti wao wenye amani.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mti wenye amani
Author - Mpumelelo Mlangeni, Tshiamo Msimanga, Tumi Mofokane
Translation - Brigid Simiyu
Illustration - Tshiamo Msimanga, Tumi Mofokane, Mpumelelo Mlangeni
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs