Maisha ya maharagwe
Nina Orange
Nina Orange

Rafiki yangu ananipatia maharagwe kutoka bustani yake.

1

Nami ninapanda haragwe moja mchangani.

2

Haragwe hilo linaota mle mchangani.

3

Mche unakua kuelekea kwenye jua.

Mzizi nao unakua ukienda chini.

4

Mche unakua na kutokezea juu ya udongo.

5

Mche huo unakua,

6

na kuzidi kua.

7

Ninapanda maharagwe zaidi.

8

Mimea hiyo inakua,

9

na kuzidi kua.

10

Mimea hiyo inazaa maganda ya mbegu.

11

Mimea hiyo inakua kuelekea juu, juu ya ukuta wangu!

12

Maganda ya mbegu yanapokauka, ninayavuna.

13

Ninakusanya mbegu kutoka kwenye maganda.

14

Ninapika maharagwe kutumia vitunguu na viungo vingine vya kutia ladha.

15

Sasa, maharagwe haya yako tayari kuliwa.

16
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Maisha ya maharagwe
Author - Nina Orange
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Nina Orange
Language - Kiswahili
Level - First words