Feni na Nyoka Kijani Kibichi
Osu Library Fund
Therson Boadu

Feni alikuwa msichana mdogo aliyekimbia kama upepo.

Feni alipenda kucheka na alijaribu alivyoweza kutenda alivyoambiwa.

1

Siku moja, Feni alienda na mama na baba kutafuta kuni.

2

Feni alipenda kumsaidia mama na baba lakini, kulikuwa na kazi nyingi za kufanya. Pia, kulikuwa na vitu vingi vya kuona: ndege, tumbili, na anga!

3

Mama alisema, "Feni! Tafadhali sikiliza! Unaweza kutafuta kuni hapa na hapo...

4

...lakini, Feni, tafadhali, chunga pahali unapokwenda, pia, kuwa mwangalifu."

5

Mama na baba wakashughulika kutafuta kuni.

6

Wakapata vipande vikubwa vya kuni.

Vilevile, wakapata vipande vidogo vya kuni.

7

Feni pia akashughulika kutafuta kuni.

Akapata vipande vidogo vya kuni.

Akapata vipande vidogo sana vya kuni.

8

Halafu Feni akatazama juu.

Akamwona ndege kwenye nyasi ndefu.

9

Kisha Feni akatazama chini. Akamwona chungu mwenye rangi ya hudhurungi.

10

Tena Feni akaliona jani maridadi. Jani hilo lilikuwa kijani kibichi na lilimetameta.

11

Feni akasema, "Hili halionekani kama jani!" Ghafla, jani hilo maridadi likasonga!

Feni akasema, "Hili si jani maridadi. Huyu ni nyoka kijani kibichi!"

12

Feni akapiga kelele, "Eii!" Feni akakimbia haraka kuwatafuta baba na mama.

13

Feni akamwona babake. Feni akasema, "Nyoka! Nyoka!"

Baba akauliza, "Wapi? Wapi?"

Feni akajibu, "Hapo! Hapo!"

14

Halafu babake akamfukuza yule nyoka kijani kibichi kwa kijiti.

Nyoka kijani kibichi akatoroka akaenda zake.

15

Baba akasema, "Feni, uko salama. Twende tumwambie mama kuhusu yule nyoka kijani kibichi."

16

Mama akasema, "Feni, nimefurahi kwamba nyoka kijani kibichi hakukuuma...

17

...lakini wakati mwingine, tafadhali, tafadhali, kuwa macho na utazame unakokwenda."

Na huo ukawa ndio mwisho wa jambo hilo.

18
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Feni na Nyoka Kijani Kibichi
Author - Osu Library Fund
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Therson Boadu
Language - Kiswahili
Level - First sentences