Pahali pangu pa furaha
Summayya Muamba
Summayya Muamba

Hadithi hii inanihusu mimi na Makao ya Watu Wazee.

1

Makao hayo ni jumba kubwa lililoko mtaani Bertrams, Johannesburg.

Nyuta zake ni za rangi rangi. Ni jumba safi lakini ndani kuna kimya. Watu wanaoishi humo ni wakongwe mno.

Siku moja mamangu alitutembeza huko.

2

Makao haya ya Watu Wazee ni pahali pangu pa furaha!

Ninafurahi niwaonapo watu wazee na kuweza kuwasaidia.

3

Siku moja nilitembelea pahali hapo na kuziosha nywele za baadhi ya wale wazee.

4

Pia, niliwaandalia chakula.

Baadhi ya wazee wale waliogofya, hata hivyo, nilifurahia kuwa pale.

5

Kulikuwa na bi kizee mmoja ambaye hakutaka kusaidiwa na yeyote.

Alianza kupiga mayowe.

6

Vilevile, kulikuwa na bi kizee mwingine aliyenikatalia nilipomshika. Mikono yake ilikuwa laini na joto.

Aliitwa Aisha, kama dadangu.

7

Watu wazee hunifurahisha.

Wana hadithi za kale ambazo sitawahi kujua.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Pahali pangu pa furaha
Author - Summayya Muamba
Translation - African Storybook
Illustration - Summayya Muamba
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs