Kuna mvulana anayeitwa Rodney. Anaishi na familia yake. Mamake ni Jemima na babake ni Mike. Dada zake ni Suzy na Lola. Rodney ni kitinda mimba.
Rodney anapenda kucheza mchezo wa chesi. Anaupenda sana hata anapokuwa akicheza, haongei.
Siku moja, Rodney alikuwa shuleni akicheza chesi. Aligundua kwamba mchezo wa chesi ungelinganishwa na familia yake.
Mike ni Mfalme. Jemima ni Malkia, ndiyo sababu ana nguvu. Suzy na Lola ni majamadari na maaskofu. Rodney ni kitunda kwa sababu ni mdogo kwa wote.
Baada ya kugundua hivyo, Rodney alikwenda nyumbani mbio kuwaelezea familia yake.
Mwanzoni, wote walimcheka. Lakini, baadaye walielewa. Rodney aliwaelezea majukumu yao na kwa nini yeye alikuwa kitunda.
Rodney alimwambia mamake kuwa yeye ni malkia, na kwamba babake ni mfalme. Dada zake ni majamadari na maaskofu.
Rodney ni kitunda kwa sababu anapenda kutalii! Angechagua kuwa chochote alichotaka, hata kama angejinyima vitu fulani.