

Miaka milioni moja iliyopita, kito cha soka kiliundwa.
Kilipogunduliwa, watu walipigana kukimiliki kito hicho chenye nguvu.
Wakati wa vita vya soka vya kwanza vya dunia kito hicho kilipotea. Hakuna aliyeelewa.
Muda ulipita. Kito hicho cha soka kilipatikana tu alipozaliwa nyota maarufu zaidi wa soka.
Si kitambo sana, kulikuwa na mvulana aliyeitwa Daudi. Alitoka katika familia maskini.
Kabla babake Daudi kufariki, alimpatia mwanawe kito hicho cha soka.
Mwanzoni, Daudi hakujua nguvu za kito hicho.
Daudi alikuwa bado kijana alipokitumia kito hicho kucheza soka.
Hakuwa ameanza kwenda shuleni. Lakini, kwa nguvu za kito hicho, Daudi alishinda kila mechi aliyocheza na marafiki zake.
Daudi alitambua kuwa angeipatia familia yake fedha kwa kucheza soka.
Angemfungulia mamake duka, na kuwapeleka kakake na dadake shule.
Daudi alijitokeza kuwa mchezaji wa soka maarufu zaidi aliyewahi kuonekana.
Hata ilisemekana kwamba alitoka ulimwengu tofauti!
Daudi ni nyota wa soka ambaye hatasahaulika kamwe!

