Mtumbwi wa Sarai
Little Zebra Books
Rachel Greer

Sarai ana mtumbwi.

Mtumbwi wake ni mkubwa.

Mtumbwi huo uko kando ya mto.

1

Baadhi ya wanawake wanafika mtoni. Mwanamke mmoja ana uteo wa matunda. Mwingine ana kuku. Mwingine ana mbuzi mmoja. Wa mwisho ana mbuzi wawili.

Wanamwuliza Sarai, "Tutavukaje mto?"

Sarai anasema, "Ingieni mtumbwi wangu!"

2

Kisha, wanaume wanafika. Mmoja ana samaki.

Mwingine ana baiskeli.

Mwingine ana gunia la mahindi.

3

Mwanamume mwingine ana magunia mawili ya mahindi.

Wanamwuliza Sarai, "Tutavukaje mto?"

Sarai anawajibu, "Ingieni mtumbwi wangu!"

4

Wanyama pia wanakuja. Wanamwuliza Sarai, "Tutavukaje mto?"

Sarai anasema, "Ingieni mtumbwi wangu!"

5

Wanyama wanaingia mtumbwini. Mbwa anaingia mtumbwini. Paka anaingia mtumbwini.

Tumbili anaingia mtumbwini. Sungura anaingia mtumbwini. Kasa anaingia mtumbwini. Swara anaingia mtumbwini.

6

Tembo anawasili kando ya mto. Anauliza, "Nitavukaje mto?"

Sarai anasema, "Ingia mtumbwi wangu!"

Tembo anaingia mtumbwini. Mtumbwi unafurika maji.

7

Salaala!

Mtumbwi umepinduka!

8

Mtumbwi huu ni mdogo sana.

Hauna nafasi ya kuwatosha wote.

9

Sarai anasema, "Hebu! Kwanza, nitawavukisha wanawake."

10

"Kisha niwavukishe wanaume," Sarai anasema tena.

11

"Hatimaye, nitawavukisha wanyama," Sarai anakamilisha maelezo yake.

12

Tembo anasema, "Heri nitembee tu!"

13
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mtumbwi wa Sarai
Author - Little Zebra Books
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Rachel Greer
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs