Vitu ninavyojua
Ursula Nafula
Michael Nakuwa

Hii ni manyatta.

Ni nyumbani kwetu.

Iko katika Kaunti ya Turkana.

1

Huyu ni ngamia.

Katika Kaunti ya Turkana, watu wanafuga wanyama tofauti.

Lakini ngamia ni muhimu mno.

2

Hawa ni walimu wangu. Ninapenda kwenda shuleni.

Shule yangu inaitwa Lolupe. Nampenda sana mwalimu wangu wa Sanaa.

3

Hii ni meli kubwa. Meli zinatumika kusafirisha watu na mizigo majini.

Nikienda Mombasa, nitaweza kuona meli.

4

Hiki ni kitanda. Ninapenda kitanda babangu alinitengezea.

Nakitumia na ndugu yangu mdogo. Ni kizuri.

5

Huyu ni jogoo. Tuna jogoo wawili nyumbani.

Tunao pia kuku wengi. Kuku hutaga mayai mengi.

6

Huyu ni panya. Panya ni wanyama hatari.

Hula chakula. Huharibu nguo pia.

Huweza kusababisha ugonjwa.

7

Huyu ni mbwa. Mbwa hufugwa.

Mbwa wetu anaitwa Daa. Hubweka sana.

8

Mwavuli huu mkubwa ni wa wazazi wangu. Ni wa rangi ya kisambarau, kimanjano na kijani kibichi.

Tunautumia inaponyesha ili tusinyeshewe.

9

Niko darasa la pili na ninajua vitu vingi. Nataka kujua vingine zaidi.

Nisivyojua, nawauliza wazazi wangu au mwalimu wangu.

10
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Vitu ninavyojua
Author - Ursula Nafula
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Michael Nakuwa
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs