Mojo na Kobe
Monica Oyovwevotu Dale
Edwin Irabor

Hapo zamani, ndege aliyeitwa Mojo aliishi katika ufalme wa Baro. Kobe alikuwa rafikiye.

Mojo alikuwa mjumbe na alisafiri mbali kupeleka jumbe.

1

Siku moja, Mfalme Simba alimwita Mojo.

Mfalme Simba alimtaka apeleke ujumbe wa maana kwa Jamaa yake, Smba Marara, aliyekuwa mfalme kwenye ufalme tofauti.

2

Kobe aliposikia hivyo, alimwonea wivu.

Alimshauri Mojo, "Usiende. Ni mtego. Simba anakutuma wewe kama kafara."

3

Mojo aliogopa. Siku iliyofuata, alienda kwa jamaa yake Jimbi akamwambia alivyoambiwa na Kobe.

Jimbi hakumwamini Kobe.

4

"Nitakutayarishia mlo mtamu usiku wa leo," Kobe alimweleza Mojo alipokutana naye baadaye.

Mojo alienda nyumbani kwa Kobe kwa furaha kwa mlo.

5

Mojo alipokuwa akistarehe, Kobe alimtupia wavu akamnasa! Kisha alienda nje kutafuta kuni.

Mojo hakuweza kusonga. "Nisaidie, nisaidie!" alilia.

6

Jimbi alikuwa karibu na nyumba ya Kobe. Alimsikia Mojo akipiga kelele. Aliita, "Mojo? Mojo?"

"Jimbi! Njoo uniokoe!" Mojo alijibu.

Jimbi alienda kwa haraka mahali Mojo alikuwa.

7

Jimbi alimwokoa Mojo kutoka kwenye wavu.

Mojo alimshukuru Jimbi kisha akikimbia na kwenda zake.

Mojo alimwambia Mfalme Simba kuhusu jambo hilo. Mfalme alimfukuza Kobe kutoka kwenye ufalme wake.

8
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way:
Mojo na Kobe
Author - Monica Oyovwevotu Dale
Translation - Ursula Nafula
Illustration - Edwin Irabor
Language - Kiswahili
Level - First paragraphs